Watakaoanza Simba hawa hapa

Muktasari:

Mazoezi ya mwisho ya Simba yamekamilika muda huu katika uwanja wa Al Hilal ya hapa Khartoum Sudan.

SUDAN

Mazoezi ya mwisho ya Simba yamekamilika muda huu katika uwanja wa Al Hilal ya hapa Khartoum Sudan.

Mazoezi hayo ya Simba ambayo yalifanyika kwa saa moja tu, kuanzia saa 8:30 mchana mpaka saa 9:30 mchana kwa saa za hapa Sudan.

Wachezaji wa Simba hawakufanya mazoezi mengi magumu wala kukimbia bali ni yale machache tena mepesi mepesi.

Miongoni mwa mazoezi ambayo walilifanya walikimbia mbio za mwendo wa kawaida na walizunguka uwanja mara mbili, mazoezi ya viungo, utimamu wa akili na mengine machache.

Zoezi la mwisho ambalo Simba walifanya la kucheza timu mbili na hapo Mwanaspoti lilibaini wachezaji ambao wanakwenda kuanza katika kikosi cha kwanza.

 Manula/Kakolanya

Katika eneo la makipa Aishi Manula alianza kufanya mazoezi mengi ya kutosha na baada ya muda alipumzika.

Akabaki Benno Kakolanya na Ally Salim wakiendelea na mazoezi kwa maana hiyo ikitokea, Manula hayupo sawa anaweza kuanza Kakolanya.

 Shomary Kapombe

Katika eneo la beki wa kulia Kapombe alipewa nafasi ya kuanza na alifanya mazoezi mengi ya kukaba na kuzuia.

 Mohammed Hussein

Beki wa kushoto anapewa nafasi ya kuanza na mazoezi yake yalifanana na Kapombe.

 Joash Onyango

Alipewa nafasi ya kumkata Meddie Kagere na John Bocco na yupo katika kikosi cha kwanza.

 Pascal Wawa

Kama ilivyokuwa kwa Onyango nae alipewa majukumu kama hayo.

 Taddeo Lwanga

Ataanza katika cha kwanza katika nafasi ya kiungo mkabaji akimpora namba Jonas Mkude.

 Clatous Chama

Anaanza katika kikosi cha kwanza atacheza kama winga wa kulia ila atasaidia zaidi katika eneo la kiungo.


 Mzamiru Yassin

Atakuwa sehemu ya kikosi cha kwanza anaanza kama kiungo mshambuliaji lakini atakuwa akimsaidia Lwanga kukaba.


 Chriss Mugalu

Mfungaji wa bao katika mechi ya ugenini dhidi ya As Vita anaanza katika kikosi cha kwanza.

 Larry Bwalya

Atakuwa nyuma ya straika kurahisha kupata mipira na kutengeneza mashambulizi ya mara kwa mara.

 Luis Miquissone

Mfungaji wa bao katika mechi iliyopita dhidi ya Al Ahly ataanza katika kikosi cha kwanza atakuwa akimsaidia Tshabalala kukaba pia.

Wakati mwingine alionekana Mkenya, Francis Kahata akiingia na kutoka kwenye nafasi hii.