Wenye hela zao!

Muktasari:

LIGI Kuu England ni moja ya michuano yenye pesa nyingi kwenye ulimwengu wa michezo.

LONDON, ENGLAND. LIGI Kuu England ni moja ya michuano yenye pesa nyingi kwenye ulimwengu wa michezo.

Ikitokea umemwaga wino kwenye klabu ya Ligi Kuu England, umejihakikishia mkwanja wa kutosha kabisa kupitia mishahara na bonasi za kila wiki. Na jambo hilo limefanya kuwapo na mastaa kibao wanaovuna mkwanja mrefu kwenye mikikimikiki hiyo ya Ligi Kuu England.

Hii hapa orodha ya mastaa watano watano wanaolipwa mkwanja mrefu kwa kila nafasi ya uwanjani kwa wale wanaopiga mzigo kwenye Ligi Kuu England.


Makipa

5.Jordan Pickford (Everton) - Pauni 100,160 kwa wiki

4.Kasper Schmeichel (Leicester City) - Pauni 130,000 kwa wiki

3.Alisson Becker (Liverpool) - Pauni 137,500 kwa wiki

2.Kepa Arrizabalaga (Chelsea) - Pauni 150,000 kwa wiki

1.David de Gea (Man United) - Pauni 375,000 kwa wiki


Mabeki wa kulia

5.Nathaniel Clyne (Crystal Palace) - Pauni 80,769 kwa wiki

4.Aaron Wan-Bissaka (Man United) - Pauni 90,000 kwa wiki

3.Reece James (Chelsea) - Pauni 91,667 kwa wiki

2.Kyle Walker (Man City) - Pauni 110,000 kwa wiki

1.Hector Bellerin (Arsenal) - Pauni 110,000 kwa wiki


Mabeki wa kushoto

5.Marcos Alonso (Chelsea) - Pauni 100,000 kwa wiki

4.Conor Townsend (West Brom) - Pauni 115,000 kwa wiki

3.Lucas Digne (Everton) - Pauni 119,000 kwa wiki

2.Luka Shaw (Man United) - Pauni 120,000 kwa wiki

1.Ben Chilwell (Chelsea) - Pauni 190,000 kwa wiki


Mabeki wa kati

5.Yerry Mina (Everton) - Pauni 120,000 kwa wiki

4.David Luiz (Arsenal) - Pauni 125,673 kwa wiki

3.Cesar Azpilicueta (Chelsea) - Pauni 145,000 kwa wiki

2.Harry Maguire (Man United) - Pauni 162,775 kwa wiki

1.Virgil van Dijk (Liverpool) - Pauni 165,000 kwa wiki


Viungo wa kati

5.Tanguy Ndombele (Tottenham) - Pauni 200,000 kwa wiki

4.Thiago Alcantara (Liverpool) - Pauni 200,000 kwa wiki

3.Thomas Partey (Arsenal) - Pauni 250,000 kwa wiki

2.Paul Pogba (Man United) - Pauni 290,000 kwa wiki

1.Kevin De Bruyne (Man City) - Pauni 385,000 kwa wiki


Mawinga

5.Willian (Arsenal) - Pauni 192,308 kwa wiki

4.Marcus Rashford (Man United) - Pauni 200,000 kwa wiki

3.Mohamed Salah (Liverpool) - Pauni 200,000 kwa wiki

2.Raheem Sterling (Man City) - Pauni 300,000 kwa wiki

1.Gareth Bale (Tottenham) - Pauni 600,000 kwa wiki


Washambuliaji wa kati

5.Harry Kane (Tottenham) - Pauni 200,000 kwa wiki

4.Edinson Cavani (Man United) - Pauni 210,000 kwa wiki

3.Sergio Aguero (Man City) - Pauni 230,135 kwa wiki

2.Anthony Martial (Man United) - Pauni 250,000 kwa wiki

1.Pierre-Emerick Aubameyang (Arsenal) - Pauni 350,000 kwa wiki.