Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Benki ya CRDB na miaka minne ya huduma bora za wakala wa benkibima nchini

Mkuu wa Huduma za wakala wa BenkiBima wa Benki ya CRDB, Linda Kamuzora.

Dar es Salaam. Benki ya CRDB, mwaka huu, inasherehekea miaka minne ya utoaji huduma za waka­la benkibima tangu ilipopatiwa leseni na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA) mwaka 2021.

Benki ya CRDB ni miongoni mwa benki chache za mwanzo kupata kibali cha kutoa huduma za wakala benkibima, ila ina his­toria ya kutoa huduma hii kama dalali wa bima kwa zaidi ya miaka 10.

Benki ilibadili mfumo wa kutoa huduma za bima kama dalali hadi kuwa na dawati maalumu la ben­ki wakala bima kufuatia mabadi­liko ya kisheria ya mwaka 2019 ambayo yalizaa huduma za waka­la benkibima ikiwa na maudhui ya kuongeza wigo na upatikanaji wa huduma hizi kwa kila Mtanzania, kwa urahisi na uhakika.

Benki ya CRDB inajivunia kufa­nya kazi na kampuni za bima 11 nchini, kampuni 10 za bima ziki­wa za Tanzania Bara na Februari mwaka huu, iliongeza huduma ya ‘Takaful’ kupitia kampuni Tanzu ya Shirika la Bima Zanzibar (ZIC Takaful) ambayo inaruhusu utoa­ji wa bidhaa za bima inayofata misingi ya dini ya Kiislamu, kuka­milisha idadi ya taasisi 11.

Na hii ndiyo alama ambayo Benki ya CRDB imekuwa ikijita­hidi kuiacha katika kila bidhaa inayoileta sokoni, thamani ya hali ya juu kwa wateja wake wa hali za maisha na imani tofauti.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, Mkuu wa Huduma za Uwakala wa BenkiBima wa CRDB, Linda Kamuzora amesema kuwa wanajivunia, kwa kushirikiana na kampuni wabia, kuleta ubuni­fu na upatikanaji wa huduma za benki wakala bima zenye kukidhi mahitaji yaliyopo ya huduma za bima ndani ya kipindi cha miaka minne. Hii ikiwemo na bima za afya, vikundi n.k.

“Tuna bima za maisha zenye manufaa ya kutoa mkono wa pole kwa ajili ya vikundi hadi mtu mmoja mmoja, huduma za bima za maafa ya biashara kubwa na ndogo, bima za ushafirisha­ji mizigo, majengo, magari, mali binafsi, majengo ya biashara, za kampuni na mashirika.

Kama hiyo haitoshi tunayo bima ya kilimo, kama mtakumbu­ka kwenye sikukuu za Nanenane Mkurugenzi wetu alisema kupitia kampuni yetu tanzu, yani CRDB Insurance Company tumejikita kuleta mabadiliko katika utam­buzi wa mifugo kwa kutumia pua hivyo kuongeza ubunifu na ush­indani katika kutoa huduma ya bima ya mifugo.

Pia tunazidi kuweka nia hii hii katika bima ya mazao ifahami­kayo kama “Kijani Bima” inayo­toa malipo endapo kuna maafa katika mazao yaliyosababishwa na mvua au ugonjwa, wadudu waangamizi n.k

Jukumu letu kuu halijaishia kwenye usambazaji wa bima bali tumepewa wajibu wa mamlaka wa kutoa elimu kwa umma kuhu­su umuhimu wa kuwa na bima, upatikanaji wake na kazi yake ni nini,” amesema Linda huku aki­taja huduma za bima za afya za vikundi na watu binafsi kuwa aina nyingine ya bima ambayo inapa­tikana kupitia Benki ya CRDB.


Ukuaji wa kutoa huduma za wakala benkibima za Benki ya CRDB

Linda amebainisha kuwa kama unaweka katika asilimia za uku­aji wa sekta hiyo, basi wamekua kwa asilimia 15 ikichangiwa na mchango wa huduma za waka­la benkibima katika mapato ya ujumla ya benki hiyo.

Kulingana na ripoti ya Tira ya mwaka 2023, Benki ya CRDB, kupitia wakala benkibima ime­shika nafasi ya kwanza ikiongoza soko la huduma za bima za jum­la, ikichangia kiasi cha Sh 45.03 bilioni sawa na asilimia 31.52 ya Jumla ya Michango ya Bima (GPW) huku ikisalia nafasi ya pili katika soko la huduma za bima za maisha kwa kuchangia Sh 60.75 bilioni, sawa na asilimia 31.79 ya Jumla ya Michango ya Bima (GPW).

Amesema kuwapo katika soko la huduma za wakala benkibima kwa muda mrefu kumewahaki­kishia nafasi yao ya uongozi, ila pia kupitia matawi yetu wateja wanapata nafasi ya kuhudumiwa na kupata maelezo kuhusu hudu­ma zetu za Bima.

Hata hivyo amesema kuwa ben­ki hiyo kwa miaka mitatu mfulu­lizo imeendelea kuwa kinara wa huduma za uwakala wa bima kati­ka bima za maisha na za ujumla.

Linda amefafanua kuwa uwaka­la wa huduma za bima kwa benki, pamoja na sababu nyingine za kibiashara, zimekuja kubadili mitazamo na dhana kuhusu bima, ambapo asilimia kubwa ya watu walikuwa na imani ya kuwa bima ni wizi.

“Hii ilichangiwa na kukosekana kwa uaminifu kwa madalali wa bima ambao hapo nyuma wali­kuwa wanapokea michango ya wateja na kukaa nayo wenyewe bila kuwasilisha kwa kampuni za bima na kutengeneza migogoro baina ya wateja na kampuni hizo,” amesema zaidi.

Amesema kuwa uwepo wa huduma za bima kupitia benki umechangia kuongeza idadi ya benki nyingine kuanza kuchukua leseni na kufanya biashara hiyo na uelewa wa watu wengi kuhusu bima na faida zake.


Faida za huduma za wakala ben­kibima kupitia Benki ya CRDB

Linda ametaja faida za bima kupitia benki hiyo ni pamoja na urahisi wa upatikanaji wa bidhaa za bima kupitia mtandao wake wa CRDB wakala nchi nzima, matawi 250 yaliyotapakaa na jukwaa lake la SimBanking, kupitia njia hizi wateja wanaweza kukata bima mahali popote na wakati wowote.

Mkopo wa bima ni faida nyingine anayoipata mteja anayekata bima na CRDB. Kuto­kana na sheria kutaka mteja wa bima kulipa michango yake kwa mkupuo mmoja, kupitia benki ya CRDB, mteja anakopeshwa kulip­iwa ada yake ya bima ya mwaka mzima huku akitakiwa kurejesha kidogo kidogo ndani ya miezi 10.

“Sokoni hakuna utaratibu huo kwa kampuni nyingi kwani utat­akiwa kulipa kiwango kamili cha mwaka mzima au asilimia 70 ndani ya miezi sita, jambo lin­aloongeza makali ya gharama za bima kwa wateja ndicho kili­chotupelekea kuja na mkopo wa bima ili kuwasaidia wateja wetu waweze kumudu kupata huduma za bima kwa unafuu.

Uzoefu wa uendeshaji wa madai ya bima kwa benki yetu unampa mteja amani ya moyo juu ya uhakika wa kupata stahiki zake bila kuingia katika migogoro. Lin­da amesema ushirikiano wao na kampuni kumi na moja za bima unawapa ujasiri na nguvu ya kuhudumia wateja wake,” amese­ma na kuongeza:

“Tunapozindua bidhaa sokoni tayari tunakuwa tumeshafanya utafiti na kuhakikisha hatua zote za kisheria zimefuatwa kuanzia underwriting, madai ya bima na namna gani ya kuelewa uende­shaji wake,” ameongeza zaidi.

Amesema ubunifu ni eneo lingine la kujivunia kwa ben­ki hiyo ambapo bidhaa za bima hubuniwa kukidhi mahitaji mah­susi ya wateja wao.

Amesema kipengele cha bima kimeongezwa kwenye baadhi ya bidhaa za benki kama faida jumuishi na kuongeza thamani ya bidhaa za benki.


Wateja wanaoishi nje ya nchi

Kwa wale wanaomiliki akaunti za benki hiyo kutokea ughaibuni, wananufaika kwa bima katika akaunti zao ambapo mteja anap­ofariki hulipiwa gharama za usa­firishaji mwili na rambirambi za Sh5 milioni kwa familia ya mare­hemu, ameeleza zaidi.

Kwenye bima za vikundi, licha ya wateja wa kifurushi cha juu zaidi kulipia kiasi cha Sh 6000 kwa mwezi lakini anaweza kupa­ta rambirambi ya hadi Sh10 mili­oni pale mwanachama au mwenzi anapofariki huku pia wakiwa na fursa ya kuongeza wanakikundi wengine. Faida zingine ikiwepo na fao la Maisha kwa kufiwa mto­to hadi wanne, fao la ulemavu wa kudumu utokanao na ajali, fao la Maisha wazazi pamoja na wakwe n.k.


Bima kidijitali na ubunifu

Katika kufanikisha mkakati wa benki kutoa huduma zake kidi­jitali, Linda amesema Benki ya CRDB inaendelea kuimarisha kuuza bidhaa za bima kupitia mfumo wa SimBanking.

“Tumeunganisha mifumo yetu ya benki na ile ya Mamlaka yaani TIRA na TRA na hivi sasa wateja wetu wanaweza kununua hudu­ma za bima, kwa mfano bima za magari kupitia SimBanking. Mteja anapolipia muamala wake unakwenda kuonekana katika mfumo wa Taifa wa kuhakiki bima.”

Linda ameweka wazi matama­nio yao kama benki ni kuende­lea kufungamanisha huduma za upatikanaji wa bima kimtandao (dijitali) zaidi kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia ya kila siku huku aki­gusia ushindani kuto­ka kwenye kampuni za mitandao ya simu.

“Tumeona hivi sasa mitandao ya simu ime­kuja na huduma tofauti zikiwemo hudu­ma za bima ambazo wate­ja wanaweza kuzipata mahala popote, hivyo kama benki tuna­jaribu kuten­geneza bidhaa zitakazozin­gatia urahisi wa upatika­naji wake na usasa kuhi­mili ushin­dani huo na kubakia kiongozi wa huduma hizi sokoni,” amesema Linda ambaye amekiri uwezekano wa hilo kupitia mtandao wao mpana wa mawakala na SimBanking.


Matarajio

Benki inaendelea na hatua ya mwisho ya kuleta bidhaa mpya ya bima sokoni ambayo inatara­jiwa kuzinduliwa hivi karibuni. Hata hivyo, amesema bidhaa hiyo itakwenda kuleta masuluhisho ya mahitaji yote ya huduma za bima kwa watu na tasisi.

Linda amesema wanatarajia kuendelea na mageuzi ya kidiji­tali kwa kutumia bidhaa zile zile huku mtazamo wao ukiwekwa zaidi katika bidhaa za bima ndo­go ndogo kwa watu wa kipato cha chini. Hii ni pamoja na kuhakiki­sha muendelezo wa kutoa taarifa na kuelimisha umma juu ya faida ya Bima.

“Mwaka jana tulianzisha bima ya buku, lengo likiwa kuongeza ukataji bima kwa watu wa mai­sha ya kawaida kabisa na kulifikia kundi hilo ambalo hukosa fursa ya kupata huduma za kifedha mara nyingi, tupo kwenye zoezi la kui­boresha huduma hii kuongezea wigo zaidi na kuwafikia Watanza­nia wengi ili kuendelea kuchagia upatikanaji wa bima.”