Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Franone Mining and Gems LTD (FMG) yasaidia jamii Simanjiro

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Franone Mining & Gem Ltd (FMG), Onesmo Mbise (kushoto) akizungumza na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma (kulia) mara baada ya ziara yake katika mji mdogo wa Mireran hivi karibuni.

Kampuni ya Franone Mining & Gem Ltd (FMG) inayochimba madini ya Tanzanite kwenye kitalu C na D, inamilikiwa na wawekezaji wazawa.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Onesmo Mbise anasema yeye na wenzake Francis Matunda na Vitus Ndakize wanamiliki asil-imia 84 na Serikali inamiliki asilimia 16 ya eneo la Kitalu C.

Kwa mujibu wa meneja mkuu wa kampuni ya FMG, Vitus Ndakize kampuni hiyo imetoa ajira rasmi 328 na ajira zisizo rasmi 1,000.

Ndakize anasema ajira zisizo rasmi zimejumuisha wauza bidhaa za chakula na huduma, mama lishe, wachekechaji na madereva wa pikipiki za kubebea abiria (bodaboda).

Kusaidia jamii

Kampuni ya Franone Mining LTD imelenga kufanikisha ujenzi wa miundombinu ya thamani ya Sh38 milioni kwenye shule ya sekondari ya kidato cha sita ya Naisinyai.

Mkurugenzi wa kampuni ya Franone Mining LTD, Onesmo Mbise anataja changamoto zitak­azotatuliwa na kampuni hiyo kwa gharama hizo ni kuchimba kisima cha maji, nishati ya umeme wa nyumba ya walimu, bweni la wasi­chana na bwalo na jiko la kudumu kwani lililopo lipo wazi linaingiza vumbi na kuchafua vyakula.

Mkuu wa shule ya sekondari ya kidato cha sita ya Naisinyai, William Ombay amemshukuru Mbise kwa kupitia kampuni yake kuka­milisha baadhi ya changamoto zin­azowakabili.

“Tunashukuru kwa kusaidia shule yetu kwani Serikali imejita­hidi kwa kiasi kikubwa kutimiza mahitaji ya shule ila wadau wa elimu kama ninyi siyo vibaya kusaidia pia,” anasema Mwalimu Ombay.

Diwani wa kata ya Naisinyai, Taiko Laizer anasema watampa ushirikiano wa kutosha mwekez­aji mzawa Onesmo Mbise kupitia kampuni ya Franone Mining LTD inayochimba madini ya Tanzanite.

“Hii ni hatua nzuri ya mahu­siano mema ya uwekezaji kupitia kampuni yako ya Franone Mining LTD na jamii ya kata ya Naisinyai, tunatarajia tutashirikiana vyema,” anasema Taiko.

Wadau waipongeza kampuni ya Franone

Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Has­san Juma, hivi karibuni amewa­ongoza wajumbe 163 wa Baraza la Wawakilishi, Mawaziri watatu na manaibu mawaziri watano wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutembelea mgodi wa kampuni ya Franone Mining LTD eneo la kitalu C.

Naibu Spika Mgeni, akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga ameongoza msafara huo kutembelea mgodi wa Kitalu C wa kampuni ya Franone Mining and Gems LTD uliopo mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro.

Akizungumza baada ya kutem­belea eneo hilo ameipongeza kam­puni ya Franone Mining and Gems LTD pamoja na uwekezaji wao pia kwa kutoa ajira 328 wakiwemo wanawake.

Anasema wamejifunza mengi ikiwemo uchimbaji wa madini ya Tanzanite unavyofanyika na kuona ukuta unaozunguka migodi ya madini hayo uliojengwa kip­indi cha uongozi wa hayati John Magufuli.

"Kule Zanzibar tunazungumzia uchumi wa bluu kupitia bahari, tumekuja hapa Franone na kuji­funza namna uchumi wa migodi unavyonufaisha Watanzania hasa wanawake," anasema Spika Mge­ni.

Mkurugenzi wa kampuni ya Franone Mining and Gems LTD, Onesmo Mbise amewakaribi­sha wageni hao na kusema kuwa wanaishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwaamini wawekezaji wazawa hadi kuwakabidhi kitalu C.

Wakuu wa Wilaya za Ruangwa, Hassan Ngoma na Nachingwea Mohamed Moyo mkoani Lindi, nao hivi karibuni wamewaongoza baadhi ya viongozi wa Wilaya zao, kutembelea na kuingia ndani ya mgodi wa Franone Mining and Gems.

Ngoma, Moyo na baadhi ya viongozi hao wamezama chini ya mgodi wa mwekezaji mzawa, kam­puni ya Franone Mining and Gems LTD, eneo la kitalu C na kujionea shughuli za uchimbaji madini zinavyofanyika.

Akizungumza baada ya kuingia kwenye mgodi huo, Ngoma anas­ema lengo la ziara yao ni kujif­unza namna shughuli za uchim­baji madini ya Tanzanite unavyo­fanyika ili nao waige mazuri.

"Tumeona shughuli za uchim­baji kwa mwekezaji mzawa kam­puni ya Franone kwa kweli wanas­tahili pongezi kwa kufanya kazi kwa ufanisi," anasema Ngoma.

Anasema wilaya yao ya Ruang­wa pia kuna uwekezaji mkubwa wa baadhi ya migodi hivyo kupitia uwekezaji wa kampuni ya Franone Mining wamejifunza kupitia madi­ni ya Tanzanite.

"Uwekezaji uliopo hapa Fra­none, unapaswa kupongezwa kwani tumeshuka chini ya ardhi mgodini mita 700 kisha tukamali­za kilomita 1.2 tumeshuhudia kazi nzuri," anasema Ngoma.

Mkuu wa Wilaya ya Nachin­gwea, Mohamed Moyo ambaye naye alizama kwenye mgodi huo ameipongeza kampuni ya Franone LTD kwa kuweka miundombinu thabiti ya uchimbaji madini ya Tanzanite.

"Watanzania wanaweza tume­ona vijana wamepata ajira kwenye kampuni ya Franone na tunam­pongeza hayati John Magufuli kwa kujenga ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite," anasema Moyo.

Diwani wa viti maalum Tara­fa ya Moipo, wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Paulina Makas­eni ameipongeza kampuni ya Fra­none Mining kwa kutoa kipaum­bele kwa wanawake wanaochek­echa kwa kuwapa mchanga.

Diwani huyo Paulina anasema wamiliki wa migodi, wachimbaji na wadau wa madini ya Tanza­nite wanapaswa kuiga mfano wa kampuni ya Franone inavyowajali wanawake.

“Tunawashukuru viongozi wa kampuni ya Franone hususani Mkurugenzi wake Onesmo Mbise kwa kuwapa mchanga wanawake wachekechaji ili wajitafutie riziki zao,” anasema Diwani Paulina.

Hata hivyo, ametoa wito kwa wanawake wachekechaji kupen­dana na kuwa na umoja katika shughuli zao ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na waepuke migogoro na migongano.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania wa CCM (UWT) Kata ya Endiamtu, Claudia Dengesi anasema hatua ya kampuni ya Franone kuwapa mchanga wanawake hao inapaswa kupongezwa kwani inawanyanyua kiuchumi.

“Wanawake hivi sasa ndi­yo wanalea familia zao hivyo tumpongeze Mkurugenzi wa Fra­none, Onesmo Mbise kwa kuwa­saidia kina mama hao wachekech­aji,” anasema.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania wa CCM (UWT) Kata ya Mirerani, Johari Mwaselela amewaomba wamiliki wa migodi ya Tanzanite waige mfano wa kampuni ya Fra­none kwa kutoa mchanga wenye mabaki mengi ya madini.

Mwaselela anasema wamiliki hao wakiwapa wanawake hao udongo uliotoka kwenye buti hawatakuwa wanafanya jambo sahihi hivyo waige mfano wa Mkurugenzi wa Franone Onesmo Mbise.

Kampuni ya Franone Min­ing and Gems Ltd, pia imekipa­tia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Simanjiro Sh30 milioni kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa chama hicho.

Kutokana na hali hiyo Mwe­nyekiti wa CCM Wilaya ya Simanjiro, Kiria Ormemei Laizer ameipongeza kampuni ya Franone Mining LTD kwa kuwapatia kiasi hicho cha Sh30 milioni za ujenzi wa ukumbi huo wa chama hicho.

Kiria anasema kitendo cha kam­puni hiyo kuchangia Sh30 milioni za ujenzi wa ukumbi wa chama hicho kinastahili pongezi kubwa kwani wameonyesha moyo wa upendo kwa CCM.

“Kwa niaba ya CCM Wilaya ya Simanjiro, pokea salamu za asante na ninakushukuru kwa kutuunga mkono katika ujenzi wa ukumbi wa mikutano wa chama chetu na tutaipatia kampuni hiyo cheti cha shukrani,” anasema Kiria.

Anasema Mkurugenzi wa FMG Onesmo Mbise ameonyesha mfano mkubwa kwa wawekezaji waliopo kwenye Wilaya ya Simanjiro kati­ka kukiunga mkono chama hicho hivyo anastahili pongezi.

Pia, Meneja wa FMG Vitus Nda­kize anasema pia wapo kwenye mpango wa ujenzi wa korido ya njia ya kuingia na kutoka kwe­nye nyumba ya kuhifadhia mai­ti (mochwari) ya kituo cha afya Mirerani ila wanasubiri orodha ya mahitaji ya manunuzi ya ujenzi (BOQ) kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wila­ya ya Simanjiro.

“Katika miradi ambayo tuna­taka kuitekeleza tunasubiria Mku­rugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, atupatie barua atuambie kipaumbele cha kusaidia jamii katika eneo lake,” anasema Ndakize.

Vilevile, Meneja wa FMG Vitus Ndakize anasema pia wametoa Sh47 milioni kwa ajili ya ujen­zi wa korido ya njia ya kuingia na kutoka kwenye nyumba ya kuhifadhi maiti (mochwari) ya kituo cha afya Mirerani."Pia kampuni ya Franone tunatekeleza agizo la Waziri wa Madini Dk Dotto Biteko aliloli­toa hivi karibuni mji mdogo wa Mirerani juu ya matengenezo ya barabara ya kuelekea mgodini tumetenga Sh171 milioni kwa ajili ya matengenezo tunasubiria mkandarasi wa ujenzi apatikane ili uanze," anasema.

Waziri wa Madini aipongeza Fra­none

Waziri wa Madini Dk Dotto Biteko ameipongeza kampuni ya wawekezaji wazawa Franone Mining and Gems Company LTD, inayochimba madini ya Tanza­nite eneo la kitalu C Mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwa namna ina­vyofanya kazi kwenye eneo hilo.

Waziri Dk Biteko ameyasema hayo kwenye ziara yake mji mdogo wa Mirerani, hivi karibuni alipo­fika kuzungumza na wadau wa madini ya Tanzanite, kutembelea kitalu C na kukagua ujenzi wa jen­go la soko la madini la Tanzanite City.

Anasema kampuni ya Franone Mining and Gems Ltd, baada ya kushinda tenda na kukabidhiwa eneo la kitalu C, imefanya kazi kubwa kwa muda mfupi, kinyume cha matarajio ya watu wengi.

“Tumepata mwekezaji bora kabisa kwani aliahidi kuwa ata­anza uzalishaji miezi 18 baada ya kupewa leseni ila ndani ya miezi sita ameweza kufanikisha uzalish­aji tofauti na malengo ya awali,” anasema Dk Biteko.

Anasema kampuni ya Franone imeanza uzalishaji wa madini ya Tanzanite kwenye kipindi amba­cho Serikali inahesabu kuwa wapo kwenye usafi na kutengeneza miundombinu ya uchimbaji.

“Kampuni ya Franone Mining ilipewa mgodi ukiwa umechakaa, wakati akifanya ukarabati wa miundombinu yake ya kazi, wao wameshaanza uzalishaji, wanasta­hili pongezi,” anasema Dk Biteko.

Anasema kampuni ya Franone imetoa ajira kwa watu 328 kwa muda mfupi na bado wapo kwe­nye ujenzi wa miundombinu na Serikali inakusanya kodi kwenye madini, inapata kodi kwenye ajira hivyo iungwe mkono.

“Ni kawaida yetu tunapomuona mwekezaji ni mweusi kama sisi tunadharau badala ya kumuunga mkono, mpeni ushirikiano Mtan­zania mwenzetu na pia kuna mama wa kimasai anasema mngeleta mgeni nisingeweza kuzungumza naye kiingereza ila Onesmo Mbise hata kimasai anasikia kidogo,” anasema Biteko.

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Dk Suleiman Serera ameipongeza kampuni ya Franone kwa namna inavyosaidia ajira kwenye maeneo yanayozunguka madini ya Tanza­nite.

“Pamoja na hayo, wanawake mnaopatiwa udongo wekeni uta­ratibu wenu vizuri ili msiwe mna­gombania huo mchanga na pia vijana mnaowasumbua kina mama wanapokuwa na udongo acheni mara moja,” anasema Dk Serera.

Mbunge wa Jimbo la Siman­jiro, Christopher Ole Sendeka ameipongeza kampuni ya Franone kwa kushinda zabuni ya kuchimba madini ya Tanzanite, eneo la kitalu C.

“Ni kampuni iliyoshinda kwa sifa stahiki na wanastahili kupewa ushirikiano katika kutimiza malen­go yao ya uwekezaji wa machimbo ya madini ya Tanzanite,” anasema Ole Sendeka.

Mmoja kati ya wanawake wanaosuka kamba za manila kwenye kampuni hiyo, Nai Ley­ani amemshukuru mkurugenzi wa kampuni hiyo Onesmo Mbise kwa kuwapa ajira.

“Kwa kweli tunamshukuru Mungu kwa kupata ajira kwani hivi sasa, tunasaidiana na wanaume zetu, katika kuhudumia na kutunza familia zetu majumbani kutokana na ajira ya Franone,” anasema Nai.

Mwenyekiti wa wanawake wachekechaji Nadoiwoki Julius, anasema kampuni ya Franone Mining imewasaidia makundi manne ya wanawake, walemavu, wazee na vijana wanaochekecha udongo.

“Tuna imani kubwa na wewe Onesmo Mbise, ila tunaomba tuongezewe udongo, kwani tupo wengi na udongo ni mchache na pia nafasi za ajira zikitokea wan­awake tusisahaulike,” anasema Nadoiwoki.

Franone wamshukuru na kuponge­za Rais Samia

Mkurugenzi Mtendaji wa Kam­puni ya Franone Mining and Gems LTD, Onesmo Mbise amemshukuru na kuipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna walivyokuwa na imani kubwa na wachimbaji wazawa hadi kukub­aliwa wao kuwekeza.

“Imani huzaa imani, kutokana na imani kubwa tuliyopewa na Serikali ya awamu ya sita inay­oongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan nasi tunatoa ahadi kuwa tutatekeleza wajibu wetu ipasavyo ili kulinda heshima tuliyopewa,” anasema Mbise.

Franone yazawadiwa

Kutokana na kampuni ya FMG kutoa udongo wa kuchekecha kwa makundi maalum ya wanawake, wazee na watu wenye ulemavu, Mkurugenzi wa kampuni hiyo Onesmo Mbise amepatiwa zawa­di ya mbuzi, rungu ya heshima ya kiongozi wa kimila (mshili) na blanketi na shuka.

Diwani wa viti maalum wa tarafa ya Moipo, Paulina Makeseni anasema zawadi hizo ni upendo kwa wanawake wanaofanya kazi ya kuchekecha mchanga wenye mabaki ya madini ya Tanzanite, yanayotolewa na kampuni ya Fra­none.

“Hivi sasa uchumi wa wan­awake hawa ni mzuri hivyo waka­ona wanunue zawadi hizi ndogo ili iwe shukurani kwao na wewe utambue furaha yao kutokana na msaada mkubwa uliowapatia,” anasema Makeseni.

Diwani wa kata ya Naisinyai, Taiko Kurian Laizer akimkabidhi Onesmo Mbise rungu ya heshima ya kiongozi wa kimila (mshili) anasema wanawake hao wamem­shirikisha jambo lao naye kwa nia ya dhati akashiriki kutokanana tukio hilo kubwa kwani kampuni hiyo imewawezesha kiuchumi wanawake hao.

“Nilikuwa na majukumu men­gine ya kikazi ila nilipomaliza na kupata taarifa ya jambo hili nikaamua nije tushiriki pamoja, kwani mtu anaposema asante nasi tunapaswa kushukuru,” anasema Taiko.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) Kata ya Mirera­ni Claudia Dengesi (Mama Sonjoo) anasema wanawake hao wametoa shukrani zao kutokana na kampuni ya FMG kuwajali wakina mama.

“Tunapaswa kumshukuru mno Mkurugenzi wetu Onesmo Mbise kwani ni mtu ambaye ana utu na kuwajali wanawake, pamoja na wazee na watu wenye ulemavu,” anasema Claudia.