Madini ya Tanzanite yanavyomnufaisha Bilionea Laizer na jamii

Mchimbaji maarufu wa madini ya Tanzanite wa mji mdogo wa Mirerani wilay­ani Simanjiro mkoani Man­yara, Bilionea Saniniu Laiz­er amejenga ghala kubwa la kuhifadhi gunia 6,000 za mazao.

Bilionea Laizer anasema ghala hilo lililopo kiton­goji cha Namelock kijiji cha Naepo kata ya Naisinyai wilayani Simanjiro, litahi­fadhi mazao ambayo ata­yatumia kwa kuwauzia kwa bei elekezi ya Serikali, watu mbalimbali, taasisi na jamii ya hali ya chini.

Anasema amefanya hivyo kwa lengo la kuhakikisha chakula kinapatikana kwa uhakika na kwa wakati huku wakiuziwa kwa bei nafuu elekezi iliyotolewa na Seri­kali.

Shamba kubwa la kilimo

Bilionea Laizer pia, ame­andaa shamba la ekari 170 kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji cha mbogam­boga kwa ajili ya kuwau­zia watu kwa bei nafuu na waweze kujenga afya zao.

“Tumeshachimba visima vitatu ambavyo vipo tayari kwa kuandaa umwagili­aji wa mashamba ya mbo­gamboga kupitia umwagili­aji huo,” anasema Bilionea Laizer.

Misaada kwa jamii

Bilionea Laizer amekuwa msaada mkubwa kwa jamii inayomzunguka ikiwemo ujenzi wa shule, nyumba za ibada, taasisi mbalim­bali, Chama Cha Mapin­duzi (CCM) na watu binafsi mmoja mmoja.

Shule ya awali na msingi Saniniu Laizer ya mchepuko wa kiingereza ipo kitongoji cha Namelock kijiji cha Nae­po kata ya Naisinyai, ime­jengwa na Bilionea Laizer kwa gharama ya sh466.8 milioni na kuikabidhi Seri­kali Januari 2021.

“Nilijenga shule hiyo na kuikabidhi Serikali ambayo ninaishukuru kwani ime­boresha zaidi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kupi­tia mradi wa Boost imejen­ga madarasa mawili mapya na matundu ya vyoo,” anas­ema Bilionea Laizer.

Hata hivyo ameiomba Serikali iongeze walimu kwenye shule hiyo na pia kukamilisha bweni la kulala wanafunzi naye atajenga bwalo la chakula kama alivyoahidi kwani jiko ame­shakamilisha.

Pia, Bilionea Laizer ame­fanikisha ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Purana mtaa wa Naepo lenye uwezo wa kuchukua zaidi ya watu 1,000.

Amechimba visima kwe­nye kitongoji chake cha Namelock na ndugu na jamaa wa eneo hilo pamoja na mifugo, wanapata maji kwa karibu tofauti na awa­li kabla ya kuchimba maji hayo.

Bilionea Laizer pia amechimba visima vya maji kwenye vijiji vya Lengasti kata ya Naisinyai na kijiji cha Olchoronyori kata ya Msitu wa Tembo, ila wanatumia gharama kubwa kuvuta maji kwa ukosefu wa nishati ya umeme kwani bado kilomita 21 kufikiwa na umeme.

“Tumechimba maji ila kinachokwamisha ni umeme hivyo kusababisha tununue mafuta ya diseli lita 400 kwa siku ili kuvuta maji ni ghara­ma kubwa hivyo tunaomba Serikali ifikishe umeme ili watu na mifugo wanufaike,” anasema.

Amechangia Sh20 milioni kwa ajili ya ujenzi wa ukum­bi wa CCM Wilaya ya Siman­jiro na pia hivi karibuni kampuni yetu tumechangia Sh10 milioni kwenye taasisi ya Amani kwanza iliyopan­da mlima wa Kilimanjiro.

“Hivi karibuni wachim­baji tulikutana na Mkuu wetu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga na nikachan­gia Sh10 milioni kwa ajili ya kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan,” anasema.

Bilionea Laizer kwenye sekta ya uchimbaji ameajiri vijana zaidi ya 400 wanao­fanya kazi migodini, hivyo kuchochea ajira na kuwae­pusha vijana kukosa kazi na kuzurura mitaani.

Hospitali kwenye migodi ya Tanzanite

Bilionea Laizer amei­omba Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa­jengea zahanati, kituo cha afya au hospitali ili wachim­baji waweze kupata mati­babu na huduma za afya kwenye machimbo ya Tan­zanite.

“Mtu anaweza akapata homa ya ghafla au akajeruhi­wa mgodini wakati wa usiku inamuwia vigumu kupata matibabu kwani hakuna usaidizi zaidi ya huduma ya kwanza migodini,” anasema Bilionea Laizer.

Anasema kukiwa na hudu­ma za afya ndani ya migo­di ya madini ya Tanzanite itakuwa faida kubwa wa wachimbaji kwani watawe­za kutibiwa muda wowote hata usiku ndani ya ukuta.

“Geti la kuingia na kutokea haliwezi kufungu­liwa kila wakati hasa usiku wa manane hivyo kunawe­za kukatokea ajali au mtu akaumwa na akashindwa kutolewa ila kungekuwepo na hospitali ingesaidia,” anasema Bilionea Laizer.

Ampongeza na kumshukuru Rais Samia

Bilionea Laizer anam­pongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna alivyowekeza miundombinu ya elimu kwa jamii ya wafugaji ambao awali hawakuwa na mwam­ko wa kusoma ila hivi sasa wanapata elimu. Bilionea Laizer amesema kupitia Rais Samia jamii ya wafu­gaji wadogo na wakulima wadogo wanapata elimu kwa ukaribu tofauti na awali walipokuwa wanatembea umbali mrefu ili wakasome hali iliyosababisha wengi wao wakatae shule.

“Akili huwa haiji kama zawadi ila Rais Samia ametupa zawadi ya shule hivyo tutapata elimu, kwani kupitia shule watoto wetu watakuwa na akili na kunu­faika wao wenyewe na jamii ya wafugaji kwa ujumla,” amesema Bilionea Laizer.

Anasema hivi sasa jamii ya wafugaji ina mwamko mkubwa mno wa kupata elimu kwani tunu kubwa waliyopewa na Rais Samia hivyo watahakikisha jamii ya eneo hilo inapata elimu.

“Mungu ambariki Rais Samia na ampe maisha marefu, azidi kumpa hek­ima na busara ya kuweza kutuongoza sisi watanzania na nawaomba viongozi wa mkoa wa Manyara na wilaya ya Simanjiro wasimamie ipasavyo fedha za miradi ya maendeleo inayoletwa na Rais wetu,” anasema Bil­ionea Laizer.