Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

TARURA inavyojipambanua katika ujenzi, ukarabati wa barabara

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua Daraja la Berega, wilayani Kilosa mkoani Morogoro Agosti 2, 2024.

Sekta ya barabara ni moja ya nguzo kuu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya nchi yoyote. Barabara, kama njia kuu za usafiri, zina mchango mkub­wa katika kuunganisha mae­neo tofauti, kurahisisha usa­firishaji wa bidhaa na hudu­ma na kuboresha maisha ya watu kwa ujumla.

Sekta hii pia ina mchango mkubwa katika kuvutia uwekezaji.Wawekezaji wan­apendelea maeneo yenye miundombinu bora ya barabara kwa kuwa inawapa uhakika wa kufikisha bidhaa zao sokoni kwa wakati. Hii inachochea maendeleo ya viwanda, kilimo, na sekta zingine za uzalishaji.

Katika kuhakikisha suala la kuunganisha jamii za viji­jini na mijini kupitia baraba­ra linafanyika kikamilifu, Serikali iliunda Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).

Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff.

TARUR ilianzishwa mwa­ka wa 2017 kwa ajili ya kurahisisha usimamizi wa barabara. Uanzishwaji wa wakala huo chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali uli­tangaza mwanzo mpya wa usimamizi wa ubora wa barabara.

Barabara kama njia za kiu­chumi

Kwa Watanzania wengi, hasa asilimia 65 waishio vijijini, barabara zinazosim­amiwa na TARURA zinale­ta tofauti kati ya ustawi na umaskini. Uchumi wa nchi unaendana na ukuaji wa sekta ya kilimo, sekta inayo­changia asilimia 26 katika Pato la Taifa.

Chai, Kahawa, Mahindi, Mihogo, mazao haya yote yanategemea barabara zin­azopitika kwa ajili ya usa­firishaji kutoka shambani hadi sokoni. Bila miundom­binu ya uhakika, mazao ya wakulima yana hatari ya kuoza katika mashamba yao ambayo hayawezi kufikiwa na wanunuzi au wasamba­zaji.

Jukumu la TARURA ni rahisi lakini kubwa sana, kuhakikisha kuwa baraba­ra hizi zinaendelea kufan­ya kazi katika misimu yote ya mwaka na kwa kufanya hivyo, kudumisha maisha ya mamilioni ya watu.

TARURA imekamilisha ujenzi wa daraja linalounganisha Kata ya Minyughe na Makilawa katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Takwimu zinaonye­sha kuwa, kati ya kilomita 144,429.77 za barabara za wilaya zilizo chini ya TARU­RA, ni kilomita 3,053.26 tu (asilimia 2.11) ndizo za lami. Kilomita 38,141.21 zilizosalia ni barabara za changarawe (asilimia 26.41) na barabara za vumbi kilomita 103,235.30 (asilimia 71.48), ambazo wakati wa mvua hushind­wa kupitika. Barabara hizi, ingawa ni muhimu maten­genezo yake ni changamoto ya kudumu.

Mtendaji Mkuu wa TARU­RA Mhandisi Victor Seff anakiri ugumu huo akisema kuwa, “Kila kilomita tuna­pambana kuiboresha, lakini kila kilomita tunayoboresha hubadilisha maisha.”

Hali ya sasa ya barabara nchini

Hadi kufikia Juni 2024, hali ya barabara za wilaya ili­kuwa na maendeleo na chan­gamoto ambazo bado zin­ahitaji kufanyiwa kazi. Kati ya mtandao wote, asilimia 28.22 (kilomita 40,752.98) ziliainishwa kuwa katika hali nzuri barabara amba­zo zinaweza kuhimili shini­kizo la matumizi ya kila siku bila kuharibika. Barabara hizi ni kielelezo cha mafan­ikio ya TARURA, matokeo ya jitihada za kuzikarabati na kuziboresha kwa ajili ya matumizi ya muda mrefu.

Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff (wa kwanza kulia) akiwa na baadhi ya wataalamu wa TARURA walipotembea moja ya miradi inayotekelezwa na wakala huyo.

Hata hivyo, kilomita 52,750.18, sawa na asilimia 36.52 zimeendelea kuwa katika hali mbaya. Hizi ndizo barabara ambazo hukumb­wa na changamoto kubwa katika kipindi cha mvua za msimu ambazo husaba­bisha kushindwa kupitika kwa sababu ya matope huku asilimia 35.26 (kilomita 50,926.60) ziko katika hali ya wastani lakini bado zina­hitaji uangalizi.

Juhudi za TARURA katika mwaka uliopita zimeweze­sha maboresho ya kuvutia. Kwa mfano, mtandao wa barabara za lami uliongeze­ka kutoka kilomita 2,558.78 Juni 2023 hadi kilomita 2,743.81 kufikia Juni 2024 ongezeko la wastani la kilo­mita 185.03. Vilevile, baraba­ra za changarawe ziliongeze­ka kutoka kilomita 21,869.16 hadi kilomita 21,890.53.

Changamoto za kibajeti

Mahitaji ya bajeti ya TARURA kwa mwaka ni Sh 1.635 trilioni, lakini inapokea takribani Sh 850 bilioni tu ikiwa ni zaidi ya nusu ya kile inachohitaji. Upungu­fu huu wa kifedha ndiyo changamoto kuu ya TARU­RA na unapunguza kwa kia­si kikubwa uwezo wa kile ambacho wakala unaweza kufikia. Pamoja na vikwazo hivyo, TARURA inaendelea kusonga mbele, ikiongozwa na mpango mkakati wake wa miaka mitano (2021/22 – 2025/26) unaolenga kubore­sha mtandao wa barabara za wilaya.

Mpango huo unaeleke­za ujenzi wa barabara za lami zenye urefu wa kilo­mita 1,450.75, uboreshaji wa barabara za changa­rawe zenye urefu wa kilo­mita 73,241.57 na ujenzi wa madaraja 945. Hadi kufikia Juni 2024, TARURA ilikuwa imejenga kilomita 923.96 za barabara za lami, kuboresha barabara za changarawe zenye urefu wa kilomita 22,815.98 na kujenga mada­raja 378.

Ni mafanikio ya kuvutia, lakini kama Mhandisi Seff anavyokiri, “Tuko mbali na tunapohitaji kuwa. Pengo kati ya matarajio yetu na rasilimali zetu ni kubwa.”

Sehemu kubwa ya mtan­dao wa barabara za TARU­RA inajumuisha barabara za vumbi kilomita 99,032.93 kati ya hizo au asilimia 68.57 ya barabara zote. Barabara hizi ndizo zilizo dhaifu zaidi, ngumu zaidi kutunza na pia ndizo muhimu zaidi.

Jamii za vijijini zinazitegemea kwa kila kitu kuanzia kusafirisha mazao ya kilimo hadi kupata huduma za afya, lakini mara nyingi zinaathirika kuto­kana na mvua za msimu. Kwa TARURA, dhamira ni kuwezesha barabara hizi zipitike mwaka mzima, bila kujali hali ya hewa.

Matumizi ya teknolojia na ubunifu katika ujenzi wa barabara

Mtazamo wa TARURA kwa sasa haujumuishi tu ukarabati na matengenezo ya barabara zilizopo lakini pia matumizi ya teknolojia mpya za kibunifu amba­zo zinalenga kuwezesha matumizi ya rasilimali chache za wakala kadiri ina­vyowezekana.

Moja ya ubunifu huo ni teknolojia ya ECOROADS ambayo imetumika kati­ka Jiji la Dodoma kujenga barabara yenye urefu wa kilometa moja na katika Wilaya ya Chamwino kujen­ga barabara za kilomita 6.95. Teknolojia ya ECOZYME ni mbinu nyingine inayojarib­iwa katika Wilaya ya Itili­ma, ambapo kilomita 5.2 za barabara zinaendelea kujengwa. Teknolojia hizi hutumia nyenzo zinazopa­tikana nchini, kupunguza gharama na athari za mazin­gira.

“Tunatafuta njia za kufa­nya kazi kubwa zaidi kwa kutumia rasilimali kidogo. Hatuwezi tu kutegemea njia zilizozoeleka. Tunapaswa kuwa wabunifu na wafanisi zaidi. Barabara zetu lazima zijengwe ili zidumu,” anase­ma Mhandisi Seff.

Dhamira ya TARURA ya ujenzi wa barabara ende­levu na wa gharama nafuu haitegemei teknolojia pekee, bali wakala umewe­ka kipaumbele katika matumizi ya rasilimali za ndani kila inapowezekana, sio tu kupunguza gharama lakini pia kusaidia uchumi wa Taifa. Mkakati huu tayari umeonyesha mafanikio kati­ka miradi kama vile ujenzi wa kilomita 58.5 za barabara za lami katika mji wa Seri­kali wa Mtumba na Daraja la Berega lenye urefu wa mita 140 katika Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.

Maendeleo na changamo­to za utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu

Licha ya ufinyu wa bajeti na ukubwa wa kazi, TARU­RA imeweza kukamilisha miradi kadhaa muhimu ya miundombinu ambayo ime­badilisha sura ya mtandao wa barabara nchini. Kwa mfano Wilaya ya Kiba­ha, wakala umeweka lami kilomita 12.5 za barabara, umeboresha upatikanaji wa maeneo muhimu ya viwan­da na kukuza uchumi.

Jijini Dar es Salaam, kilo­mita 12.8 za barabara za lami zimekamilika katika eneo la Mbweni na kutoa unafuu kwa wakazi ambao hapo awali walilazimika kupita kwenye njia za udon­go zenye hali mbaya.

Moja ya mafanikio makub­wa ya TARURA ni ujenzi wa madaraja kadhaa ya chuma katika mikoa muhimu kama Kihansi-Mlimba, Ruipa-Ki­lombero na Miyuge-Ikungi. Madaraja haya yanatumika kama kiunganishi muhimu kati ya jamii za vijijini amba­zo hapo awali zilitengwa wakati wa msimu wa mvua. Daraja la Kalambo mkoani Rukwa ni mradi mwingine muhimu unaounganisha jamii na kutoa huduma muhimu kwa mwaka mzima.

Mbali na miradi hii iliyoka­milika, kuna baadhi ambayo imekwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha, jambo linalosababisha mtandao wa barabara za TARURA kuwa hatarini haswa wakati wa mvua ambao barabara za vumbi zinakuwa katika changamoto kubwa.

Jinsi TARURA inavyosaidia ukuaji wa kilimo

Mradi wa Agri-Connect ni mojawapo ya mipan­go muhimu inayolenga kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ya kimkakati ya kilimo nchini. Mradi huo wa miaka mitano uliozinduliwa mwaka 2018, umetengewa bajeti ya Sh 116.44 bilioni iliyogawanywa katika awamu tatu.

Lengo ni kuleta mabadi­liko, kuhakikisha kwam­ba wakulima walio kati­ka mikoa inayolima chai, kahawa, mbogamboga na matunda wanaweza kupele­ka bidhaa zao sokoni kwa haraka na kwa ufanisi.

Awamu ya kwanza ya mradi huo ililenga wilaya za Kilolo, Mufindi na Mbeya ili­shuhudia ujenzi wa baraba­ra zenye urefu wa kilomita 87.6 kwa gharama ya Sh 40.5 bilioni. Barabara hizi amba­zo sasa zimekamilika kwa asilimia 100 tayari zimeleta faida kubwa katika uchu­mi, zimepunguza gharama za usafirishaji na kuonge­za ufikiaji wa masoko kwa wakulima.

Awamu ya pili kwa sasa inaendelea, ambapo baraba­ra zenye urefu wa kilomita 49.12 zinaendelea kujengwa katika wilaya zote kama vile Wanging’ombe na Mbozi.

Mhandisi Seff ana matu­maini kuhusu uwezo wa muda mrefu wa mradi huo kwa kusema kuwa “Baraba­ra hizi ni zaidi ya miun­dombinu bali pia ni njia za maisha kwa wakulima wetu. Kwa kuwa na barabara bora, wanaweza kufikia masoko haraka, kupunguza ubadhir­ifu na kuongeza mapato yao.”

TARURA na mkakati wa kuziinua jamii za vijijini

Mpango mwingine muhimu ni Mradi wa Ubore­shaji wa Barabara za Viji­jini na Fursa za Kijamii na Kiuchumi (RISE). Mradi huu uliotengewa bajeti ya Sh 822.5 bilioni, umebuni­wa ili kuboresha barabara za vijijini na kutengeneza fursa za ajira. Kwa ufadhi­li wa mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dun­ia, RISE unalenga kujenga barabara za lami zenye ure­fu wa kilometa 535 (kilomita 400 ambazo zinasimamiwa na TARURA) huku ikitunza kilomita 23,000 za barabara za wilaya.

RISE tayari umean­za kuzaa matunda kwani barabara za Wenda-Mgama na Mtilili-Ifwagi katika wilaya za Iringa na Mufindi zimekamilika kwa asilimia 60 na usanifu wa baraba­ra katika wilaya nyingine muhimu kama vile Ruang­wa na Mbogwe unakaribia kukamilika.

Mradi pia unalenga ush­irikishwaji wa jamii ili huhakikisha kwamba waka­zi wa eneo hilo wanashiriki kikamilifu katika mchakato wa maendeleo, kupata ajira kuwa na umiliki wa miun­dombinu inayojengwa.

Mhandisi Seff anajivunia kile ambacho mradi wa RISE unakifanya kwa kusema “Sisi hatujengi barabara tu bali pia tunajenga mustak­abali imara. Barabara hizi huunganisha watu, huten­geneza fursa na kuinua jamii nzima.”

Mkakati wa kuboresha mae­neo ya mijini

Wakati barabara za vijijini ndizo lengo kuu la TARU­RA, wakala pia unahusika katika miradi inayolenga kuleta mabadiliko katika maeneo ya mijini yanayokua kwa kasi nchini kwa kupi­tia utekelezaji wa mradi wa Kubadilisha Miundombinu na Ushindani wa Miji Tan­zania (TACTIC) uliotenge­wa bajeti ya Sh 1.66 trilioni unaofadhiliwa kwa mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia.

Lengo la TACTIC ni kuboresha miundombinu katika halmashauri 45 za miji, ikiwa ni pamoja na miji mikuu mitano kama Arusha, Dodoma na Mwanza. Mra­di huo ulioanza mwaka wa 2022 hauangazii tu ujenzi wa barabara bali pia ujenzi wa masoko, vituo vya maba­si na mifumo ya mifereji ya majitaka. Mikataba ya awamu ya kwanza ya ujenzi ilitiwa saini mwishoni mwa 2023, na kazi tayari inaende­lea katika miji 12 na baraba­ra na mifumo ya mifereji ya majitaka ikiwa ndiyo kipa­umbele cha kwanza.

Kukabiliana na changamoto za kimazingira

Changamoto za miun­dombinu ya Tanzania haziko kwenye ujenzi wa barabara pekee bali hata mafuriko ambayo kwa muda mrefu yamekuwa suala la kudumu katika baadhi ya maeneo, hasa katika Bonde la Mto Msimbazi jijini Dar es Salaam.

Mradi wa Maendeleo ya Bonde la Mto Msimba­zi unalenga kukabiliana na suala hili, kupanua na kuongeza kina cha mto huo ili kudhibiti mtiririko wa maji na kuzuia mafuriko. Mradi huo unafadhiliwa kupitia mchanganyiko wa mikopo na misaada kutoka Benki ya Dunia, Hispania na Uholanzi.

Mradi huu hauhusu tu kuzuia mafuriko bali pia kubadilisha bonde hilo kuwa eneo jipya la kiuchu­mi. Mipango yake ni pamoja na uundaji wa hekta 57 za maeneo ya wazi na makazi pamoja na ujenzi wa Daraja la Jangwani, ambalo lita­kuwa kiungo muhimu cha usafiri wa jiji hilo. Mhandi­si Seff anaona mradi wa Msimbazi ni ishara ya kile ambacho TARURA inaweza kufikia. “Tunachukua eneo ambalo limekuwa tatizo kwa miongo kadhaa na kuligeuza kuwa mali ya jiji,” anasema.

Safari kuelekea 2025

TARURA inasonga mbele kupitia mpango mkakati wake, ikiendelea kuwe­ka malengo yaliyoainish­wa katika Ilani ya CCM ya 2020. Wakala tayari umevu­ka malengo kadhaa, ikiwa ni pamoja na upanuzi wa mtan­dao wa barabara za wilaya hadi kilomita 144,429.77 na kuvuka lengo la awali la kilo­mita 143,881. Vilevile, TARU­RA imevuka lengo la ujenzi wa barabara za changarawe na kufikia kilomita 42,059.17 sawa na lengo la 2025 la kilomita 35,000.

Lakini bado kuna kazi nyingi za kufanywa amba­po Wakala unaendelea na ujenzi wa barabara za lami unaolenga kufikia kilometa 3,337.66 ifikapo mwaka 2025 na kushirikiana kikamilifu na halmashauri ili kuhakiki­sha kuwa fedha zinatengwa kwa ajili ya matengenezo na uboreshaji wa barabara.

Dhamira ya TARURA kati­ka ubunifu pia inaendeleza mipango yake ya mbeleni. Wakala unafanyia majarib­io teknolojia mpya za ujenzi wa barabara zinazotumia nyenzo zinazopatikana nchini ili kupunguza ghara­ma na athari za kimazingira.

Miradi kama vile majarib­io ya ECOROADS na ECO­ZYME inafungua njia kwa mustakabali endelevu zaidi, ambapo barabara za Tanza­nia zitajengwa ili kudumu na zenye uwezo wa kuhimili mifumo ya hali ya hewa isiy­otabirika.

Safari ya TARURA bado inaendelea, lakini maende­leo ambayo imefikia hadi sasa hayana ubishi. Kuanzia barabara za vumbi za viji­jini hadi barabara za mijini zenye shughuli nyingi, kazi ya wakala ni kurekebisha sura ya nchi, barabara moja baada ya nyingine. Mhandisi Seff ana matumaini na mika­kati iliyopo kwa kusema kuwa “Hatujengi barabara tu, tunajenga Taifa.”

Safari ya kuelekea 2025 ni ndefu na imejaa changamo­to nyingi, lakini kadri Tan­zania inavyoendelea kukua na kustawi, TARURA nayo inaendelea kuwepo ikiten­geneza njia ya kuelekea kwenye mustakabali mzuri na endelevu. Barabara zin­aweza kuwa mbovu kwa sasa, lakini kwa kila kilomi­ta kufanyiwa kazi, Tanzania inakaribia kufikia uwezo wake kamili wa kuwa nchi iliyounganishwa na baraba­ra zenye ubora.