Wataalamu wanawake wa Yara wachangia usalama wa chakula, kipato kwa wakulima

Kutana na Mwajuma Mwangu na Veronica Rusa­gira, wataalamu wa kilimo ambao wanajinasibu kutoog­opa na kujifunga kibwebwe kushiriki katika kukuza kili­mo nchini.

Wanawake hawa wanafan­ya kazi katika kampuni ya Norway inayotengeneza na kusambaza mbolea na kemi­kali nyingine za kilimo, Yara, tawi la Tanzania. Ni wan­awake pekee katika nyadhifa zao katika kampuni hiyo.

Wakiongea na Mwananchi kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani (Machi 8, 2023), Mwajuma na Voronica wanasema wana shauku kubwa ya kusonga mbele katika shughuli wali­yoichagua.

Wataalamu hao wanatu­maini kuwa mfano kwa wan­awake wengi vijana waji­unge na shughuli za kilimo. Wanaamini kuwa mchango wa wanawake katika kuleta utoshelevu wa chakula na kupunguza umaskini ni wa muhimu. Wanataka kuona wanawake wengi wakiwa mstari wa mbele katika mny­ororo wa thamani wa kilimo.


Veronica Rusagira

Akiwa mhitimu wa Chuo cha Kikuu cha Kilimo cha Sokonine (SUA), Veronika alijiunga na Yara Tanzania mwaka 2019 baada ya kufanya kazi katika kampuni nyingine kwa muda mfupi. Wakati huo alikuwa akisimamia miradi ya kilimo cha bustani katika Mkoa wa Iringa, lakini sasa anasimamia shughuli za Yara Dar es Salaam, Mkoa wa Pwani na Zanzibar.

Kazi yake ni kuhakikisha wakulima wanapata mavuno ya kutosha ili wajipatie kipato kizuri kwa mauzo ya mazao kupitia mipango mizuri ya kilimo cha kitaalamu kama vile matumizi sahihi ya mbo­lea na virutubisho vingine.

Veronica amekulia sham­ba na tangu akiwa na umri mdogo alijifunza thamani ya kufanya kazi kwa bidii na umuhimu wa kilimo katika kuendesha maisha.

“Kazi yangu inasukumwa na dhamira ya kutaka kuona wakulima wanafanikiwa. Ni kazi nzuri. Fikiria inasisimua kiasi gani kuwasaidia waku­lima na nchi yako kuwa na chakula cha kutosha,” anas­ema.

Anasema ni muhimu kuku­za usawa wa kijinsia katika sekta ya kilimo na uelewa wa fursa mbali mbali zinazopati­kana kwa wote.

“Ni ukweli usiofurahisha kwamba wasichana wengi wanakwepa kuingia kwenye kilimo kwa sababu wanaona kilimo ni taaluma ya wanau­me,” anasema.

Anatoa wito wa kuanzish­wa kwa programu zinazowa­lenga wasichana shuleni na wanawake vijana, kukuza ushiriki wa wanawake katika kilimo na kupinga upofu wa kijinsia na mila zinazowakati­sha tamaa wanawake.

Veronica anashukuru kwamba akiwa Yara anapata msaada na ushirikiano unao­hitajika kuvuka malengo yake ya kazi na kitaaluma. Uvumilivu wa wazazi wake ndio uliomsukuma kutumia utaalamu wake kusaidia kuleta matokeo chanya kwe­nye maisha ya wakulima na kuchangia katika maendeleo endelevu.

Kwa mfano, anazungumzia furaha aliyoipata kushuhu­dia mafanikio makubwa ya mkulima aliyekuwa akimsi­mamia kupata Sh200 milioni kutoka kwenye mavuno yake ya nyanya. “Nilishawishika sana na fursa zilizoko kwenye kilimo katika kubadili maisha ya mamilioni ya wakulima na jamii zao,” anasema.


Mwajuma Mwangu

Mwajuma ambaye pia ni mhitimu wa SUA alikuwa siku zote na udadisi mkubwa kuhusu kilimo.

“Mshawishi wangu mkub­wa alikuwa mjomba wangu. Alikuwa anapata fedha nyingi kupitia kilimo na alinishawi­shi nikasomee sayansi ya uchumi wa kilimo baada ya kuona udadisi wangu katika masuala ya kilimo,” anasema.

Baada ya kufanya kazi na kampuni mbili za kahawa kwa miaka minane, alijiunga na Yara mwaka 2021 na tangu wakati huo amekuwa aki­simamia shughuli za Yara katika mkoa wa Songwe.

“Yara nimepata mazingira yanayofaa kuchangia kwa ubora wote utaalamu wa kilimo yanayogusa maelfu ya wakulima kwa kufanya kazi karibu na Serikali, wakulima na washirika wengine.”

Mwajuma alikulia katika kijiji kidogo ambapo kahawa ilikuwa ni sehemu muhimu sana ya maisha ya jamii yake. Hilo lilimfanya hata aamue kusomea Shahada ya Uzamili katika Uchumi na Sayansi ya Kahawa.

“Ndoto yangu ni kuona vijana wanafanikiwa kupitia kilimo. Nafasi ya kufanikiwa Tanzania ni kubwa, na kufan­ya kazi na watoa huduma kama Yara kunaweza kufani­kisha zaidi.”

Anasema kilimo ni muhimu kwa maendeleo endelevu. Anatumia muda mashamba­ni, akifanya kazi sambamba na wakulima, na kuwapa mipango mizuri ya kilimo na ufumbuzi kutoka Yara ambao hutolewa kulingana na mahi­taji pekee ya kila mkulima.

“Wanawake wengi zaidi watiwe moyo ili kujihusi­sha na kilimo na kushinda ubaguzi wowote wa kijin­sia, hata kwa wanataaluma kama mimi. Kama wan­awake, ni lazima tuwe na imani na uwezo wetu na tuwe tayari kutoa mawazo yetu. Unapopewa fursa lazima uoneshe unaweza kufanya, hakuna tusichoweza kufanya kama tunaiweka akili yetu katika hilo,” anasema huku akiishukuru kampuni ya Yara Tanzania kwa kumruhusu kujaribu na kuwa mbunifu katika kutoa huduma za kita­alam. Mkurugenzi Mkuu wa Yara Tanzania, Winstone Odhiambo, anasema kampu­ni ya Yara inashirikiana na serekali na wadau mbalim­bali kuwafikishia wakulima bidhaa na huduma mbalim­bali ili kuwanyanyua kimai­sha kupitia kilimo.

“Hapa Yara tuna furaha kwamba wataalam wetu wanaishi kivitendo mpango wetu wa kuilisha na kuilinda dunia, huku tukitoa ufum­buzi wenye tija kwa kilimo na mazingira,” alisema Mr Odhiambo.