Koneksheni! Ni neno ambalo limekuwa kubwa na kutambulika na watu wengi kwa maana tofauti, japokuwa wengi wanalitumia ndivyo sivyo.

Wajanja wa mjini wanakwambia unapokuwa na mtu anayeweza kukupatia koneksheni, inaleta urahisi au wepesi wa kupata taarifa nyeti kwa wakati na kufanikisha jambo lako kwa urahisi zaidi.

Miongoni mwa watu mashuhuri wanaotajwa kama daraja kwa walio wengi ni pamoja na msanii wa maigizo na mchekeshaji machachari, Steven Mengere, maarufu Steve Nyerere.