VIDEO: Nape afunguka, atetea urais wa Magufuli

Muktasari:

Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amezungumzia mambo matatu kuhusu tamko lililotolewa na makatibu wakuu wawili wa zamani wa chama hicho, Yusuf Makamba na Abdulrahman Kinana huku akisema wanaodhani Rais John Magufuli hawezi kugombea urais mwakani wanapoteza muda wao


Dar es Salaam. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amezungumzia mambo matatu kuhusu tamko lililotolewa na makatibu wakuu wawili wa zamani wa chama hicho, Yusuf Makamba na Abdulrahman Kinana huku akisema wanaodhani Rais John Magufuli hawezi kugombea urais mwakani wanapoteza muda wao.

Hata hivyo, hakuwa tayari kuzungumzia sauti zinazodaiwa kuwa za kwake zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwa madai suala hilo lina ujinai na kwamba anaviachia vyombo vinavyohusika.

Nape, ambaye amewahi kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM akizungumwa na Mwananchi jana alisema anayedhani kuna uwezekano wa kumfanya Rais John Magufuli asiwanie nafasi hiyo mwaka 2020 anajisumbua kwa kuwa utaratibu wa CCM Rais aliyepo madarakani, huwania tena nafasi hiyo awamu ya pili.

Taarifa zaidi ndani ya Gazeti la Mwananchi