Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Mama Kayai ataka kukutana uso kwa uso na Diamond

Msanii maarufu wa vichekesho nchini Kenya Mary Khavere maarufu kama Mama Kayai amesema anatamani sana kukutana na Msanii wa Tanzania Diamond Plutnumz kwa kuwa ni msanii mkubwa jambo ambalo angefurahi sana.

Mama Kayai ambaye amejichukulia umaarufu nchini Kenya katika kundi la Vitimbi  ameyasema hayo katika mahojiano na MCL DIGITAL wakati wa Tamasha kubwa la JamaFest2019 linalofanyika katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam.

Tamasha la JamaFest ni tamasha la Utamaduni la afrika mashariki ambalo linakutanisha Burudani mchanganyiko kutoka mataifa husika huku leo Jumapili Septemba 22 Msanii Diamond Plutnamz akitarajiwa kutoa burudani .