Mgonjwa mwingine wa virusi vya corona aripotiwa Zanzibar

Waziri wa Afya, Hamad Rashid Mohammed

Muktasari:

Serikali ya Zanzibar imetangaza kuongezeka kwa mgonjwa mwingine wa virisi vya corona na kufikia wawili.

Zanzibar. Waziri wa Afya, Hamad Rashid Mohammed ametangaza kuongezeka kwa mgonjwa mwingine mmoja mwenye virusi vya corona (Covid 19) na hivyo kuwa idadi ya watu wawili Zanzibar.
Hamad ameyasema hayo leo Machi 25 wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari.
Amesema mgonjwa huyo ni mwanamke na ni mke wa aliegunduliwa mwanzoni.
Hata hivyo, ameleza kuwa Serikali imetoa siku tatu kwa kufungwa safari za kwenda na kurudi Zanzibar hivyo hakuna atakayetoka wala kuingia badaa ya siku tatu kuanzia sasa.

Endelea kufuatilia Mwananchi