Dodoma. Rais Samia Suluhu Hassan anatimiza mwaka mmoja tangu achukue madaraka ya nchi, pamoja na maendeleo aliyoyasimamia amebainisha mikakati yake muhimu katika kuijenga nchi.

Akizungumza kwenye mahojiano hayo yaliyoongozwa na Bakari Machumu, Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Ltd - wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi, The Citizen, Mwanaspoti na Mwananchi Digital, Rais vilevile aliyataja mambo yaliyompa matumaini katika kuiongoza nchi kuwa ni uzoefu wake serikalini, ndani ya CCM na uwezo wa kujieleza kwa Watanzania.