Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Adaiwa kumuua dada yake, kisa fedha za nyanya

Adaiwa kumuua dada yake, kisa fedha za nyanya

Muktasari:

Mkazi wa kijiji cha Urauri ,kata ya Reha wilayani Rombo, Magreth Mushi ameuawa na kaka yake, Neoni Lazaro kwa madai ya kugombania fedha alizouza nyanya.

Rombo.Mkazi wa kijiji cha Urauri ,kata ya Reha wilayani Rombo, Magreth Mushi ameuawa na kaka yake,Neoni Lazaro kwa madai ya kugombania fedha alizouza nyanya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Ronald Makona amesema tukio hilo limetokea Februari 9, mwaka huu.

"Februari 9,mwaka huu majira ya saa tatu  katika kijiji cha Urauri Mwanamke aitwaye Magreth Mushi alijeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kichwani na kaka yake ," amesema Kamanda Makona

Ameongeza "majeruhi alipopelekwa Hospitali ya Huruma kwa ajili ya kupatiwa matibabu alifariki dunia usiku huo wa kuamkia Februari 10 mwaka huu,"

Kamanda Makona amesema mwili wa mwanamke huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti , Hospitali ya Huruma.