Dk Charles Kimei ashinda ubunge Vunjo

Dk Charles Kimei

Muktasari:

Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Vunjo, Michael Mwandezi amemtangaza Dk Charles Kimei kupitia CCM kuwa mshindi katika uchaguzi jimbo la Vunjo baada ya kupata kura 40,170.

Moshi. Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Vunjo, Michael Mwandezi amemtangaza Dk Charles Kimei kupitia CCM kuwa mshindi katika uchaguzi jimbo la Vunjo baada ya kupata kura 40,170.

Grace Kiwelu wa Chadema amepata 8,675, James Mbatia wa NCCR amepata kura 4, 949, Agustino  Mrema  kutoka TLP kura 606, Michael Salewa AAFP amepata  kura 470 na Idd Husein Act Wazalendo kura 215.

Amesema katika jimbo hilo, waliojiandikisha ni 141,864 , kura zilizozopigwa 56, 113 kura halali 55,085 kura zilizoharibika 1,028