Dk Mahera aapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Tamisemi
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo Jumamosi, Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri.
Dodoma. Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumamosi Machi 11, 2023, amemuapisha Dk Wilson Mahera kuwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.
Kabla ya uteuzi huo uliofanya hivi karibuni, Dk Mahera alikuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Katika uteuzi huo, Rais Samia alimteua Ramadhan Kailima aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu- Tamisemi kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tume ya Taifa ya Uchaguzi.