Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Helkopta yatumika kuua nzige

Helkopta yatumika kuua nzige

Muktasari:

  • Waziri wa Kilimo  nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda na naibu wake, Hussein Bashe wameweka kambi usiku wa kuamkia leo Jumatano  Machi 3, 2021 eneo la Engaruka  wilayani Monduli Mkoa  wa Arusha kusimamia shughuli ya kuteketeza nzige wa jangwani.

Monduli. Waziri wa Kilimo  nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda na naibu wake, Hussein Bashe wameweka kambi usiku wa kuamkia leo Jumatano  Machi 3, 2021 eneo la Engaruka  wilayani Monduli Mkoa  wa Arusha kusimamia shughuli ya kuteketeza nzige wa jangwani.

Helkopta ya shirika la kupambana na nzige wekundu ambalo makao makuu yake ni nchini Zambia leo asubuhi imeanza  kunyunyiza dawa kuwaangamiza nzige hao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Profesa Mkenda amesema kazi waliyonayo ni kuangamiza kundi la nzige walioingia Wilaya ya Monduli.

"Leo tuko hapa eneo la Engaruka kuongeza kasi ya kuwaangamiza nzige, kama tumemaliza kuwaangamiza nzige hawa Simanjiro tukiweza kupiga sumu leo na kesho tutalimaliza kundi hili na kazi itakayobaki ni kushughulika upande wa Kenya ili nzige hawa wasiingie tena.”

"Nawashukuru sana wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa Wilaya kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa na leo tumelala hapa na helkopta hii itaendelea kubaki hapa mpaka tutakapohakikisha hata yai moja la nzige hakuna," amesema Profesa Mkenda

Maeneo ambayo awali nzige hao walivamia wakitokea  nchini Kenya na kuangamizwa ni Wilaya za Siha, Mwanga na Simanjiro.

Februari  19, 2021 katibu mkuu wa wizara  hiyo, Gerald  Kusaya amesema lipo kundi la nzige zaidi ya milioni 50 walioingia nchini kupitia Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.