Hotuba ya kwanza ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

#Live​: Samia Suluhu Hassan kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania, historia mpya yaandikwa

Muktasari:

  • Leo Ijumaa Machi 19, 2021 Samia Suluhu Hassan ameapishwa kuwa Rais wa sita wa Tanzania.

Leo Ijumaa Machi 19, 2021 Samia Suluhu Hassan ameapishwa kuwa Rais wa sita wa Tanzania.

Hafla ya kuapishwa kwake imefanyika Ikulu Dar es Salaam na kuweka historia ya kuwa rais wa kwanza mwanamke nchini Tanzania.

Samia amechukua nafasi ya aliyekuwa rais wa Tanzania,  John Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 kwa maradhi ya moyo katika hospitali ya Mzena alikokuwa akipatiwa matibabu.