Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ilichokisema Serikali ya Tanzania kuhusu wawekezaji

Ilichokisema Serikali ya Tanzania kuhusu wawekezaji

Muktasari:

Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda  amewataka wawekezaji wa ndani  kutumia fursa ya uhitaji wa pembejeo   kuongeza uzalishaji.

Babati.Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Profesa Adolf Mkenda  amewataka wawekezaji wa ndani  kutumia fursa ya uhitaji wa pembejeo   kuongeza uzalishaji.


Amesema kwa sasa Serikali inaagiza takribani tani 700,000 za mbolea nje ya nchi.

Alieleza hayo jana Jumamosi Aprili 17, 2021 alipofanya ziara katika  kiwanda cha mbolea cha Minjingu kilichopo Wilaya ya Babati kuangalia shughuli za uzalishaji zinazoendelea katika kiwanda hicho.

"Sasa hivi tunataka pembejeo zipatikane kwa wakulima kwa gharama nafuu na kwa wakati, mahitaji yetu ya pembejeo tutumie kama fursa ya kuongeza uzalishaji ndani ya nchi yetu."

"Tuongeze kasi ya uzalishaji ili hii mbolea ambayo tunaagiza nje  iweze kuzalishwa hapa Minjingu, tunataka vya kwetu kwanza ili mradi vinakuwa na viwango vinavyotakiwa na kwa bei nafuu ambayo mkulima anaweza kumudu," amesema Profesa Mkenda.

Amewaalika wawekezaji  wanaotaka kuja nchi kuwekeza kwenye pembejeo na kwamba Serikali itasimama nao na kuwapa upendeleo.
"Tunawaalika wawekezaji popote walipo waje wazalishe mbolea hapa nchini,  hatutajali uraia wake tutampa upendeleo maalumu ,tutawalinda na tutasimama nao,"amesema Profesa Mkenda.