Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

LIVE: The Citizen Rising Woman 2026

LIVE: The Citizen Rising Woman 2026

Dar es Salaam. Wadau wakiwamo wanawake zaidi ya 400 kutoka sekta mbalimbali nchini, wakishiriki Jukwaa la Sita la The Citizen Rising Woman Initiative (RWI) linalofanyika muda huu katika Ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam.

Jukwaa hili linafanyika ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa kila ifikapo Machi 8 na kaulimbiu yake inasema isemayo: “Give to Gain: Elevate Her Rise,” ikimaanisha:  “Toa ili Upate: Inua Safari ya Mafanikio ya Mwanamke.”

Jukwaa hili linaloandaliwa kila mwaka na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), huwakutanisha wanawake na wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili uwezeshaji wa wanawake, kubadilishana uzoefu na kujenga mitandao ya kitaaluma.