Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Muuguzi anayedaiwa kumbaka mjamzito asimamishwa kazi

Muktasari:

Emmanuel Mpanduji, muuguzi wa zahanati ya kijiji cha Luganga wilayani Mbogwe Mkoa wa Geita anayedaiwa kumbaka mjamzito amesimamishwa kazi.

Mbogwe. Emmanuel Mpanduji, muuguzi wa zahanati ya kijiji cha Luganga wilayani Mbogwe Mkoa wa Geita anayedaiwa kumbaka mjamzito amesimamishwa kazi.

Akizungumza leo Alhamisi Januari 23, 2020 kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Samwel Makala amesema amefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.

Muuguzi huyo yupo rumande baada ya kusomewa mashtaka ya kubaka katika mahakama ya wilaya ya Mbogwe na kukosa dhamana.

“Tayari tumemsimamisha kazi wakati kesi yake ikiendelea mahakamani na uchuguzi zaidi unafanyika,” amesema.