Mwanamke akutwa amejinyonga Kilimanjaro
Muktasari:
- Maria Sigarai (26) mkazi wa kijiji cha Kwalakamu wilayani Rombo amekutwa amejinyonga huku mwili wake ukining’inia kwenye mti.
Rombo. Maria Sigarai (26) mkazi wa kijiji cha Kwalakamu wilayani Rombo amekutwa amejinyonga huku mwili wake ukining’inia kwenye mti.
Tukio hilo limetokea Machi 11, 2021 kwenye moja ya shamba lililopo karibu na kijiji hicho.
Kaimu Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Ronald Makona amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na uchunguzi wa kifo cha mwanamke huyo aliyeacha mtoto wa umri wa miezi minne.
"Machi 11 mwaka huu katika kijiji cha Kwalakamu kata ya Kitirima tarafa ya Usseri wilayani Rombo alikutwa amefariki baada ya kujinyonga kwenye mti kwa kutumia kamba ya katani.”
"Chanzo cha kujinyonga hakijafahamika na uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea, mwili umehifadhiwa katika hospitali ya Karume ,"amesema Kamanda Makona.