Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Polisi kuchunguza madai askari kugeuza simu za wizi mradi binafsi

Muktasari:

  •  Jeshi la Polisi nchini limeanza kufanyia kazi habari ya uchunguzi ya gazeti la Mwananchi kuhusu baadhi ya askari wake kugeuza simu za wizi kuwa mradi wao binafsi kwa kuchukua fedha kwa watu waliopoteza au kuibiwa simu.



Dar es Salaam. Jeshi la Polisi nchini limeanza kufanyia kazi habari ya uchunguzi ya gazeti la Mwananchi kuhusu baadhi ya askari wake kugeuza simu za wizi kuwa mradi wao binafsi kwa kuchukua fedha kwa watu waliopoteza au kuibiwa simu.

Katika taarifa yake jeshi hilo limesema, "Jana Novemba  katika  moja ya magazeti ya hapa nchini ilitolewa taarifa yenye kichwa cha habari " Askari wageuza simu za wizi mradi binafsi. Hata  leo Novemba 30 gazeti hilo pia limeandika taarifa nyingine yenye kichwa cha habari 'Mapya yaibuka askari kugeuza simu za wizi mradi binafsi'.

Jeshi la polisi lingependa kutamka kwamba kuanzia jana  taarifa hiyo ilianza kufanyiwa uchunguzi wa kina wa kubaini askari hao wachache wanaofanya vitendo hivyo."