Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

RC Mghwira aeleza wadudu waliovamia kijiji walivyodhibitiwa

RC Mghwira aeleza wadudu waliovamia kijiji walivyodhibitiwa

Muktasari:

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema wadudu wanaodaiwa kuwa ni nzige walioonekana katika kijiji cha Karamandei kata ya Toloha  wilayani Mwanga  walidhibitiwa.

Moshi. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema wadudu wanaodaiwa kuwa ni nzige walioonekana katika kijiji cha Karamandei kata ya Toloha  wilayani Mwanga  walidhibitiwa.

Ameeleza  hayo leo Alhamisi Februari 18, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Moshi.

"Kulitokea wimbi la nzige Wilaya ya Mwanga  uongozi wa Wilaya uliwahi kuijulisha wizara ambayo ilisaidia mapema na bado wanaendelea kuangalia kama kuna dalili zozote za kurudi lakini mpaka leo asubuhi sijaletewa taarifa kama bado nzige wapo au wanaendelea kuleta madhara yoyote."

Kuhusu madhara ya nzige hao amesema walivamie eneo la msitu lenye majani na walibaki eneo hilo.