Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Serikali kugharamia mazishi waliofariki ajalini Tanga

Muktasari:

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amesema Serikali itagharamia mazishi ya familia ya watu 17 waliofariki kwa ajali ya gari wilayani Korogwe mkoani Tanga.



Tanga. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Omary Mgumba amesema Serikali itagharamia mazishi ya familia ya watu 17 waliofariki kwa ajali ya gari wilayani Korogwe mkoani Tanga.

Ajali hiyo ilitokea jana usiku katika eneo la Magira Gereza, wilayani hapo barabara ya Segera-Buiko na kusababisha vifo hivyo pamoja na majeruhi 12.

Ndugu hao walikuwa wakisindikiza mwili wa mwanafamilia mwenzao, Athanas Mrema (59) aliyefariki dunia Februari Mosi, kutoka Dar es Salaam kuelekea mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza leo Jumamosi Februari 4, 2023 katika Hospitali ya Magunga wilayani hapo amesema Serikali itagharamia mazishi ya familia hiyo.