Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Serikali yaeleza haja ya kufungamanisha mfumo wa Mahakama na Kimila

  • Mwakilishi wa Mwanasheria Mkuu Mkoa Kilimanjaro Tamari Mndeme, akizungumza leo katika maadhimisho ya Siku ya sheria nchini.

Muktasari:

  • Imeelezwa kuwa mfumo wa kimila hurahisisha mchakato wa kutoa haki na hivyo utawezesha kuharakisha mashauri mahakamani. 

Moshi.  Mwakilishi wa Mwanasheria mkuu wa serikali mkoani Kilimanjaro Tamari Mndeme  amesema kuna haja ya kufungamanisha mfumo wa kisheria unotumiwa na Mahakama na mfumo wa kimila au kiasili katika utoaji wa haki ili kupunguza mlundikano wa mahabusu gerezani.
Mndeme ameyasema hayo leo Februari Mosi wakati Mahakama Kuu ikiadhimisha kutimiza miaka 100, ya utendaji wake nchini ikiwa pia ni siku ya maadhimishi siku ya sheria nchini. 
Akizungumza katika maadhimisho hayo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, Mndeme amesema zipo faida nyingi katika kutatua migogoro kwa kutumia  taratibu au  falsafa za  kimila na kiasili  ikiwepo  kuunganisha jamii  husika.
Amefafanua  kuwa gharama katika utatuaji wa migogoro kwa njia ya asili ni ndogo ikilinganishwa na  mfumo wa sasa wa mahakama  ambapo hutumia gharama kubwa kutokana na kuwepo  kwa changamoto mbalimbali  ikiwepo kuleta mashahidi,  kufungua mashauri, na kuweka mawakili
"Mfumo huu wa asili  hutumia muda mfupi  ikilinganishwa na mfumo wa sasa ambapo  baadhi ya mashauri yanakaa muda mrefu  na mwisho kuleta msongamano wa mahabusu  magerezani hasa kwa makosa yale yasiyokuwa na dhamana".
Amefafanua  kuwa  serikali ilifanya juhudi kubwa  kuingiza mfumo wa kimila  ya utoaji haki, katika sheria ya matumizi ya sheria sura ya 358 ya sheria ya Tanzania ambayo inaruhusu matumizi ya  ya sheria za kimila  pale ambapo wahusika wa migogoro  wanatoka katika jamii iliyojiwekea  mfumo  wa  utatuzi wa migogoro.