Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tamwa yatoa pole kwa waathirika wa vurugu

Muktasari:

  • Chama hicho kimeendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda utu, kuheshimu haki za kila mmoja na kudumisha mazungumzo ya amani kama nguzo muhimu ya Taifa.

Dar es Salaam. Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa) kimeeleza huzuni na kutoa pole kwa Watanzania wote waliopata madhila kutokana na vurugu zilizotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Vurugu hizo zilitokea wakati uchaguzi ukiendelea nchini jambo lililosababisha uharibifu wa mali za umma, binafsi pamoja na vifo.

Taarifa iliyotolewa leo Novemba 5, 2025 kwa umma na Mkurugenzi Mtendaji wa Tamwa, Dk Rose Reuben, imeeleza kuwa pole maalumu zinatolewa kwa familia zote zilizopoteza wanawake, watoto, na wanahabari, pamoja na wale wote walioumia au kuathirika kwa namna yoyote kutokana na matukio hayo ya kusikitisha.

“Wakati Taifa likipitia katika kipindi kigumu katika hali hii, tunaiunga mkono familia na jamii zote zinazojitahidi kuijenga upya hali ya utulivu, mshikamano na amani nchini,” imeeleza taarifa hiyo ya  Dk Reuben.

Chama hicho kimeendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda utu wa binadamu, kuheshimu haki za kila mmoja na kudumisha mazungumzo ya amani kama nguzo muhimu ya Taifa.

 Tamwa inasisitiza kuwa, kulinda amani na mshikamano ni jukumu la kila Mtanzania, ili kuondoa hofu na kuimarisha mshikamano wa kijamii.

“Tunaendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda utu, kuheshimu haki za binadamu na kudumisha mazungumzo ya amani kama nguzo ya Taifa letu,” amesema Dk Reuben kupitia taarifa hiyo.