Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tanzania kutengeneza magari, bajaji zisizohitaji dereva

Mkurugenzi wa Tehama Tanzania, Dk Nkundwe Mwasaga

Unguja. Katika mkakati wa kukuza Tehama na Ubunifu nchini, Tanzania imealika kampuni 15 za Misri, huku lengo likiwa kuhakikisha katika miaka michache ijayo, Tanzania itengeneze magari na bajaji za umeme na zisizo hitaji dereva.

Akizungumza katika maonyesho ya biashara baina ya wafanyabiashara wa Zanzibar na Misri mjini Unguja leo Julai 18, 2023, Mkurugenzi Mkuu Tume ya Teknolojia Habari na Mawasiliano Tanzania (ICTC), Dk Nkundwe Mwasaga amesema Tanzania ina wabunifu wengi.

“Tanzania kuna kampuni ambazo zina ubunifu utakaosaidia kutengeneza magari yanayotumia umeme na tayari kuna watu wameonyesha uwezo huo hivyo kuja kwa kampuni hizo itakuwa fursa ya kuendelza ubunifu huo,” amesama na kuongeza;

“Sasa ili kukuza Tehama na Ubunifu nchini, ICTC imezialika kampuni kubwa 15 za Tehama kutoka nchini Misri kukutana na kampuni za hapa nchini kubadilisha uzoefu na hivyo kuviwezesha vyuo nchini kujenga hayo magari.”

Kwa mujibu wa Dk Nkundwe, magari hayo yatakuwa yanaendeshwa bila kuwa dereva na kwamba mwakampuni hayo yaliyoalikwa wana teknolojia hiyo lakini pia wana ile inayohusu matumizi ya betri ambazo hazitumii umeme mkubwa.

“Na kama uhusiano huu utaendelea vizuri, basi kwa mara ya kwanza Tanzania inaweza kuwa na bajaji na magari yanaendeshwa bila kuwa na dereva, huku yakitumia umeme mdogo, lengo letu ni Tehama nchini,” amesema.

Hivyo Dk Mwasaga amewataka kampuni na watu binafsi wenye ubunifu katika Tehama kuhakikisha wanachangamkia fursa hiyo kupata uzoefu zaidi kukuza Tehama nchini

Naye Meneja Mkuu wa Benki ya Misri, Emad Shawky, amesema ni wakati sasa kati ya kampuni za Tanzania na Misri kushirikiana kukuza biashara na uchumi wa mataifa hayo mawali.

Ofisa kutoka Tantrade ambayo inashirikiana na Fredy Liundi amesema hiyo ni fursa kati ya mataifa hayo mawili kwahiyo watapata uwezo mkubwa kubadilishana uwezo hata kufungua viwanda hapa nchini.