Wabunge waliotimuliwa uanachama Chadema watinga bungeni

Muktasari:

  • Wabunge wa viti maalum waliofukuzwa uanachama wa Chadema juzi leo Ijuma Mei 13 wameudhuria vikao vya Bunge isipokuwa Halima Mdee na Ester Bulaya.

Dodoma. Wabunge wa viti maalum waliofukuzwa uanachama wa Chadema juzi leo Ijuma Mei 13 wameudhuria vikao vya Bunge isipokuwa Halima Mdee na Ester Bulaya.

Aliyenza kuingia ndani ya ukumbi wa Bunge ni Ester Matiko saa 2:50 asabuhi akifutiwa na Salome Makamba na wengine waliingia baadaya kikao cha Bunge kuanza.

Leo kila mmoja na wakati wake, tofauti na mara ya kwanza walipofika kwa ajili ya kuapishwa ambapo waliingia wote 19 katika viwanja vya Bunge.

Hadi kufiki saa tatu Bunge linaanza wabunge watatu na wengine waliingia baada ya kikao cha leo kuanza.

Wabunge wengine waliingia baada ya kikao kuanza huku wabunge wengine wakiwa wametulia kama kawaida.