Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wana CCM 19 wajitokeza kumrithi Kwandikwa Ushetu

Wana CCM 19 wajitokeza kumrithi Kwandikwa Ushetu

Muktasari:

  • Wanachama 19 wa CCM wamechukua fomu za kuwania kuteuliwa kuwa wagombea ubunge katika jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga.

Kahama. Wakati uchukuaji wa fomu wa kuwania ubunge katika jimbo la Ushetu mkoani Shinyanga ukikamilishwa, wanachama 19 wa CCM wamejitokeza, wanaume wakiwa 17 na wanawake wawili.


Uchaguzi wa jimbo hilo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Elias Kwandikwa aliyefariki dunia Agosti 2, 2021 jijini Dar es Salaam.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Septemba 1, Mkurugenzi wa uchaguzi wa CCM, Emmanuel Mbamange amesema, wanachama wote waliochukua fomu wamerejesha kwa wakati na hakuna fomu iliyoharibika.


Amewataka wagombea hao kuwa ni  Samson Lutonja, Makoye Mayengo, James Lembeli, Bundala Shija, Paschal Michael, Emmanuel Charahani, Yohana Masonda, Ernest Nila, Ahmed Haroun, Betha Juma, Mhandisi Manyango Nchambi, Marry Lema, Erhard Mlyasi na Dk Mathew Masele.

Wengine ni pamoja na Dk Lameck Makoye Nyaligwa, Marthin Mwakatundu, Makwaya Michael, Jorodani Balindo pamoja na Profesa Simon Julius Maziku.


Hata hivyo, Mbamange amesema kazi inayofuata ni upigaji wa kura za maoni utakaoshirikisha wajumbe halali wa chama hicho 880 na kwamba mgombea atakayeshinda atakuwa bado hajateuliwa mpaka atakapothibitishwa.


Amesema jimbo hilo linawapiga kura 165,418 na kuwasisitiza wagombea kutojihusisha na vitendo vya rushwa.

Kwa upande wake katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Donald Magessa amesema kuwa, maandalizi ya kupiga kura za maoni kwa watia nia yamekamilika na uchaguzi huo utafanyikia katika ukumbi wa sekondari Dakama wilayani humo.