Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Zimamoto wauzima moto jengo la Tamisemi Dodoma

Muktasari:


  • Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma  limeuzima moto uliodumu kwa saa kadhaa na kuteketeza baadhi ya sehemu ya jengo la ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).







Dodoma. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dodoma limeuzima moto uliodumu kwa saa kadhaa na kuteketeza baadhi ya sehemu ya jengo la ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Mto huo ulianza saa 11  jioni na ilipofika  saa 1 usiku jeshi hilo lilikuwa limefanikiwa kuuzima.

Wakizungumza na Mwananchi Digital mashuhuda wa tukio hilo wamesema moto huo ulianza kwa kasi huku Rashid Mazrui akieleza kuwa  alikuwa akiingia msikiti wa Nunge kwa ajili ya kufanya ibada lakini alipoangalia upande wa pili aliona moshi ukitoka katika jengo la Tamisemi.

“Nikaacha kwenda kuswali na kuanza  kuangalia kuna nini nikaona wafanyakazi wakikimbia kuomba msaada, tukaanza kuwasaidia kuwatoa nje,” amesema.

Maimuna Shaaban mfanyakazi wa Tamisemi amesema moto huo ulianza kama mzaha na walifanya juhudi za kuuzima lakini walipoona unazidi walilazimika kupiga simu Zimamoto.

“Tunashukuru wamefika kwa wakati na wanaendelea kuuzima kama unavyoona,” amesema.