Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wakongwe England wamshambulia Thomas Tuchel

Meneja wa England, Thomas Tuchel

Muktasari:

  • Gareth Southgate aliiongoza England kucheza hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia mara moja na pia kucheza Fainali ya Kombe la Euro mara mbili.

Nyota wawili wa zamani wa timu ya Taifa ya England, Wayne Rooney na Kyle Walker, wamesema kuwa kichapo cha mabao 2-1 ambacho timu hiyo imekipata kutoka kwa Argentina katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026 jana Julai 15, 2026 ni matokeo ya mipango mibovu ya Meneja wa England, Thomas Tuchel.

Licha ya England kutangulia kupata bao kupitia kwa Anthony Gordon katika dakika ya 55, Argentina ilisawazisha katika dakika ya 85 kupitia kwa Enzo Fernandez na kisha kupata bao la ushindi katika dakika za majeruhi lililofungwa na Lautaro Martinez.

Lawama nyingine zimeelekezwa kwa Tuchel hasa kwa uamuzi wake wa kuirudisha timu nyuma kujilinda baada ya kutangulia kufunga bao na pia kufanya mabadiliko ya kuingiza idadi kubwa ya mabeki.

Wayne Rooney amesema kuwa Thomas Tuchel alikuwa "anajitafutia matatizo" kwa mabadiliko ya wachezaji aliyofanya dhidi ya Argentina.

"Tulijiweka katika nafasi nzuri sana, lakini hatukujua tufanye nini baada ya hapo. Tulirudi nyuma na kuwapa nafasi ya kutushambulia. Walituwekea presha kubwa, na hatimaye tukavunjika. Mara tu walipopata bao la kwanza, ilikuwa wazi kwamba wangepata la pili pia.

"Unapokuwa juu ya mpinzani, unapaswa kuendelea kubaki juu yake. Tunafunga bao la kuongoza 1-0, halafu tunarudi nyuma, tunafanya mabadiliko, tunaweka wachezaji watano au sita kwenye safu ya ulinzi. Ukimruhusu Lionel Messi na Argentina wakushambulie kwa uhuru, unakuwa unajitafutia matatizo," amesema Rooney.

Walker kwa upande wake amesema kuwa hakuna cha maana ambacho Tuchel anakifanya ndani ya kikosi cha England kulinganisha na mtangulizi wake, Gareth Southgate.

"Gareth alituongoza hadi nusu fainali ya Kombe la Dunia na kufika fainali mbili za Mashindano ya Ulaya (EURO). Huenda sasa watu wakaanza kuthamini kile alichokifanya na kutambua jinsi ilivyo vigumu kuvuka hatua hiyo na kutwaa ubingwa katika mashindano yoyote.

Hiki ndicho kisa kilekile ambacho nimekiona kwa miaka kumi ya mwisho ya maisha yangu ya soka. Daima kumekuwa na 'kama', 'lakini' na 'pengine' kila timu ya England inapocheza.

Bado tunaendelea kuwa miongoni mwa timu zinazopewa nafasi ya kushinda, lakini kuwa mshindani pekee hakutoshi. Tunapaswa kuwa mabingwa. Kucheza fainali ya Kombe la Dunia Jumapili kungekuwa jambo la kujivunia na sherehe kubwa kwa taifa zima," amesema Walker.

Walker amesema kuwa Tuchel hawezi kukwepa lawama kwa kilichotokea jana.

"Lakini tumefika katika hatua fulani, tumefanya mambo yale yale tuliyokuwa tukiyafanya nilipokuwa bado nacheza, na mwisho wake tumepata matokeo yaleyale.

"Ni lazima tuangalie mabadiliko ya wachezaji yaliyofanywa wakati wa mchezo. Siwezi kulikwepa suala hilo. Pia kocha anapaswa kujitathmini kuhusu maamuzi aliyofanya katika kufanya mabadiliko hayo," amesema Walker.