WAKATI sherehe za kilele cha 'Wiki ya Mwananchi' ikihitimishwa leo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Mwananchi Digital ipo live eneo hilo kukuletea matukio yote muhimu yanayoendelea kuanzia muda huu hadi masaa ya mechi.

Yanga inahitimisha 'Wiki ya Wananchi' leo ikiwa ni msimu wa nne tangu kuanzishwa kwake huku ikitarajia kucheza mchezo wa kirafiki na mabingwa wa Ligi Kuu ya Uganda, Vipers utakaopigwa saa 1:00 usiku.