Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga amesema wamezuia vifaranga 62, 730 vya kuku wa mayai kuingia nchini baada ya kubainika kutokuwa na vibali pamoja na cheti cha afya.

Vifaranga hivyo ambavyo ni mali ya kampuni ya Phoenix Farms Limited ya Mkuranga mkoani Pwani vilivyohifadhiwa katika makasha 697 vilikuwa vinatokea Ubelgiji na vimezuiliwa katika uwanja ndege wa Julius Nyerere eneo la mizigo.