Kilichotokea kwenye sherehe ya Ali Kiba acha tu!

Muktasari:

  • Katika sherehe hizo, Kiba aliingia ukumbini hapo na ndugu yake, Abdu Kiba aliyekuwa amevalia pia nguo aina ya joho pamoja na rafiki yake, Ommy Dimpoz wote ni wasanii wa Bongo Freva lakini yeye alipigia suti kali ya rangi nyekundu na nyeusi.

Mombasa. KIMASOMASO mwanangu usimwone, ni wimbo ambao Ali Kiba alimwimba mkewe, Amina Khalef mara tu baada ya kumkumbatia wakati wa sherehe yao iliyofanyika jana Alhamisi kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee mjini Mombasa.

Kiba ambaye alivalia nguo aina ya Joho na kilemba cheupe alimwimbia mrembo wake huyo ambaye 

usiku huo alikuwa kama malaika kutokana na namna alivyopendeza na gauni lake refu lililokuwa na rangi ya krimu na limejimwaga kama manyoya ya ndege Tausi.

Baada ya hapo, alianza kucheza naye muziki laini aina ya bluzi taratibu na nderemo na vifijo vikasikika watu wakishangilia si unajua kelele za akina mama tena wanapokuwa na yao na mambo yakaendelea.

Ikafika wakati wa kumtafuta baba unajua ilikuwaje, si akatajwa Gavana Hassan Joho 'Sultan' ambaye aliwasili ukumbini hapo mapema.

Katika sherehe hizo, Kiba aliingia ukumbini hapo na ndugu yake, Abdu Kiba aliyekuwa amevalia pia nguo aina ya joho pamoja na rafiki yake Ommy Dimpoz wote ni wasanii  wa Bongo Freva lakini yeye alipiga suti kali ya rangi nyekundu na nyeusi.