Samatta uso kwa uso na Pepe, azikwepa Arsenal, Chelsea

Muktasari:

  • Safari ya kwenda Baku, Azerbaijan itakapochezwa fainali Mei mwakani imeanza rasmi baada ya kupangwa kwa makundi hayo leo.

Monaco, Ufaransa. Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta atakuwa na kibarua kizito mbele ya beki mkongwe wa Ureno, Pepe baada ya Genk kupangwa Kundi I pamoja Besiktas, Malmo na Sarposborg katika mashindano ya Europa Ligi.

Mabao matano ya Samatta yameisaidia Genk kufuzu kwa hatua ya makundi, lakini sasa anategemea kupata upinzani mkali kutoka kwa Pepe anayesifika kwa kucheza soka la kibabe wakati Genk itakapowavaa Besiktas ya Uturuki inayopewa nafasi kubwa ya kumaliza kinara wa kundi hilo.

Nyota wengine wa Besiktas watakaowapa wakati mgumu Genk ya Samatta ni kiungo Mreno Ricardo Quaresma na Ryan Babel aliyewahi kutamba na Liverpool.

Mbali ya Besiktas pia Genk itakuwa na kibarua kutoka kwa timu za Scandnavia Malmo ya Sweden pamoja na Sarposborg ya Norway.

Samatta amesema hofu juu ya vigogo watakao kutana nao kwenye hatua hiyo ya makundi ambayo itaanza kuchezwa, Septemba 20.

Nahodha huyo wa Taifa Stars, amekuwa gumzo katika vyombo mbalimbali vya habari barani Ulaya kutokana na kiwango alichokionyesha kwenye michezo ya kuwania kutinga hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Safari ya kwenda Baku, Azerbaijan itakapochezwa fainali Mei mwakani imeanza rasmi baada ya kupangwa kwa makundi hayo leo.

Arsenal, Chelsea, Sevilla, AC Milan, Bayer Leverkusen na Lazio ni timu zinazopewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo.

Arsenal yenyewe ipo Kundi E pamoja na Sporting Lisbon (Ureno), Qarabag (Azerbaijan) na Vorskia (Ukraine).

Chelsea imetupwa Kundi L pamoja na PAOK (Ugiriki), Borisov (Bulgaria) na Vidi (Hungary).

Makundi

Kundi A: Leverkusen, Ludogorets, Zurich, Larnaca

Kundi B: Salzburg, Celtic, Leipzig, Rosenborg

Kundi C: Zenit, Copenhagen, Bordeaux, Slavia Prague

Kundi D: Anderlecht,Fenerbahce, Dinamo Zagreb

Spartak Trnava

Kundi E: ARSENAL, Sporting Lisbon, Qarabag, Vorskla Poltava

Kundi F: Olympiacos, Milan,Real Betis, Dudelange

Kundi G: Villarreal, Rapid Vienna, Spartak Moscow, Rangers

Kundi H: Lazio, Marseille, Frankfurt, Apollon

Kundi I: Besiktas, GENK, Malmo, Sarpsborg

Kundi L: CHELSEA, PAOK, BATE Borisov, MOL Vidi

Kundi K: Jablonec, Dynamo Kiev, Astana, Rennes

Kundi J: Sevilla, Krasnodar, Standard Liege, Akhisar