Vitamini A ya kwenye kiazi inapunguza kasi ya kuzeeka

Muktasari:

  • Viazi vitamu vinastawisha mwili hasa ngozi bila kujali ni ya mwanamke au mwanaume hasa vile visivyowekewa vinasaba kwa lengo la kuongeza kiwango chake cha vitamin A ya asili.

Viazi vitamu ni miongoni mwa vyakula vya wanga vyenye faida mwilini kwa sababu vina viini lishe na dawa lishe zinazoweza kukinga na kutibu baadhi ya maradhi.

Viazi vitamu vinastawisha mwili hasa ngozi bila kujali ni ya mwanamke au mwanaume hasa vile visivyowekewa vinasaba kwa lengo la kuongeza kiwango chake cha vitamin A ya asili.

Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Chakula na Dawa, Marekani (U.S. FDA) imebainisha kiazi kimoja kikubwa kinaweza kumpatia mtu asilimia 100 ya Vitamini A inayohitajika mwilini kila siku.

Unapokula viazi vitamu unapata vitamin A, C , B5, B6, C, E na unapata madini ya potasiumu, magneziamu, fosforasi, manganese, zinki, wanga, sukali ya asili, nyuzi lishe, beta- carotene na choline zinazosaidia kustawisha ngozi ya mwanadamu na kuifanya nzuri na husaidia mtu kupata usingizi mzuri.

Taasisi ya Afya ya Marekani (NIH) inasema Vitamini A inayopatikana kwenye viazi inasaidia kupunguza kasi ya kuzeeka na inaimarisha afya ya macho.

Hata hivyo, Daktari bingwa wa macho kutoka Hospitali ya Duke, Jill Koury anasema upunguvu wa Vitamini A unasababisha sehemu ya jicho inayopokea mwanga kuharibika na kusababisha uoni hafifu. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Kitivo cha Sayansi ya Lishe cha Harvard, Shule Kuu ya Afya ya Jamii (HSPH), beta-Carotene inapunguza uwezekano wa kupata saratani ya utumbo na tezi dume.

Pia, dawa lishe aina ya beta-Carotene inayopatikana kwenye viazi husaidia kudhibiti maradhi ya moyo, pumu na kupunguza kasi ya mwili kuchakaa.

Utafiti huo pia ulibainisha dawa lishe hiyo huwasaidia wanawake kutengeneza vichocheo muhimu wakati wa ujauzito na kunyonyesha huku madini ya potasiamu yaliyopo ndani ya viazi hivyo inasaidia kupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la damu.

Vinasaidia kuondoa madini yasiyohitajika mwilini, kuboresha ufanyaji kazi wa moyo, kuboresha mapafu, kuimarisha kinga ya mwili na ni chanzo kikubwa cha beta-carotene. Faida nyingine ni chanzo cha madini ya chuma, potassium na calcium,