Rais JPM awaapisha mawaziri wapya
Muktasari:
Mawaziri walioapishwa leo ni Profesa Palamagamba Kabudi,aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba na Harrison Mwakyembe aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Dar es Salaam. Rais John Magufuli amewaapisha mawaziri wawili aliowateua hivi karibuni katika hafla fupi iliyofanyika leo Ikulu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali.
Mawaziri walioapishwa leo ni Profesa Palamagamba Kabudi,aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba na Harrison Mwakyembe aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Profesa Kabudi anaenda kuongoza wizara iliyokuwa ikiongozwa na Dk Mwakyembe
Wakati Mwakyembe anashika nafasi ya Nape Nnauye aliyebadilishwa hivi karibuni.