VIDEO: Chidi Benzi adaiwa kukutwa na gramu tano za Bangi
Muktasari:
Kamanda Muroto amesema kuwa Chidi benz atafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.
Dodoma. Polisi mkoani Dodoma inamshikilia mwanamuziki wa Hip Hop Chidi Benzi kwa tuhuma za kukutwa na bangi gramu tano.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 18, Kamanda wa polisi Dodoma Gilles Muroto amesema Chidi Benz amekamatwa mwishoni mwa wiki katika eneo la mji Mpya Jijini Dodoma.
Kamanda Muroto amesema kuwa Chidi benz atafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.
Soma Zaidi: Chid Benz adakwa tena na dawa za kulevya
Miongoni mwa nyimbo zilizompa umaarufu Chid Benz ni pamoja na Ngoma Itambae, Mmenisoma, Naitwa Nani, Hasira za Nini na Mashallah.
Soma Zaidi: Chid Benz anaswa na dawa za kulevya ‘airport’