Kiwanda cha sukari cha Magereza kuzalisha tani 30, 000 kwa mwaka
Muktasari:
Jeshi la Magereza limefufua kiwanda hicho na shamba la miwa la Gereza la Mbigiri mkoani Morogoro.
Dar es Salaam. Kiwanda cha sukari cha Jeshi la Magereza kilichokuwa kimefungwa mwaka 1996 kinatarajia kuzalisha tani 30, 000 kwa mwaka baada ya kuanza tena uzalishaji.
Jeshi la Magereza limefufua kiwanda hicho na shamba la miwa la Gereza la Mbigiri mkoani Morogoro.
Akizungumza wakati Magereza wakisaini mkataba wa makubaliano na mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na PPF, kupitia Kampuni Tanzu ya Mkulazi Limited, Mkurugenzi Mtendaji wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara alisema kazi ya ukaguzi na ya kitaalamu imeshafanyika na tani 30,000 za sukari zitazalishwa kwa mwaka.