Lema atoka hospitalini

Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema ameruhusiwa kutoka hospitali ya Aga Khan alikolazwa jana kwa matibabu baada ya kutoka mahakamani alikosomewa mashtaka katika kesi mbili za uchochezi.

Muktasari:

Akizungumza na Mwananchi, Lema amesema ililazimika kupelekwa hospitali kutokana na kuona ana matatizo ya kiafya hasa kutokana na kufunga kula siku tatu na vurugu zilizotokea jana mahakamani.

Arusha. Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema ameruhusiwa kutoka hospitali ya Aga Khan alikolazwa jana kwa matibabu baada ya kutoka mahakamani alikosomewa mashtaka katika kesi mbili za uchochezi.
Akizungumza na Mwananchi, Lema amesema ililazimika kupelekwa hospitali kutokana na kuona ana matatizo ya kiafya hasa kutokana na kufunga kula siku tatu na vurugu zilizotokea jana mahakamani.
"Nimepata ruhusa, nipo nyumbani naendelea vizuri lakini  natarajia kuandika barua ya Malalamiko kwa Jaji Mkuu na Msajili wa mahakama  kuelezea vurugu zilizotokea juzi," amesema.