M/kiti wa CCM mkoa wa Kigoma afariki dunia

Muktasari:

Akitoa taarifa ya kifo chake, msemaji wa familia, Amon Ndinande amesema merehemu alikuwa anasumbuliwa na kisukari na shinikizo la damu, hali iliyosababisha kupata ugonjwa wa kiharusi

Kigoma. Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa Kigoma, Samson Naingo (76) amefariki dunia akiwa anapata matibabu katika hospitali ya rufaa mkoa wa Kigoma, Maweni.

Akitoa taarifa ya kifo chake, msemaji wa familia, Amon Ndinande amesema merehemu alikuwa anasumbuliwa na kisukari na shinikizo la damu, hali iliyosababisha kupata ugonjwa wa kiharusi.

Amesema kabla ya kufikwa na mauti marehemu alilazwa hospitali ya Maweni alipokuwa akipatiwa matibabu, kuanzia Februari 10 mwaka huu hadi alipofariki dunia.

Naingo aliitumikia CCM kwa miaka 20 akiwa kiongozi wa wilaya ya Kasulu na mkoa wa Kigoma.