Magufuli awapitia wanafunzi 4,450

Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jaffo

Muktasari:

Akizungumza juzi na watumishi wa halamshauri za Mji, Ushetu na Msalala, Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jaffo alisema idadi hiyo inachangiwa na maofisa elimu kushinda ofisini bila kwenda kuzikagua.

Kahama. Sekondari katika halmashauri tatu za Wilaya ya Kahama, zimebainika kuwa na wanafunzi hewa 4,445.

Akizungumza juzi na watumishi wa halamshauri za Mji, Ushetu na Msalala, Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jaffo alisema idadi hiyo inachangiwa na maofisa elimu kushinda ofisini bila kwenda kuzikagua.

“Tatizo hili linatokana na maofisa elimu kushinda ofisini, kwani hawapati takwimu sahihi za idadi ya wanafunzi na matokeo yake wakiulizwa, wengi wao hutoa takwimu za makadirio,” alisema Jaffo.

Aliwataka watumishi hao kutojiona miungu watu katika maeno yao, bali watembelee shule na kuwathamini wafanyakazi waliopo chini yao.