Mahakama yataka kujua upelelezi kesi ya Aveva, Kaburu

Muktasari:

  • Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa alieleza hayo baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kudai upelelezi bado haujakamilika.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka katika kesi inayomkabili   Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na makamu wake, Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu kueleza upelelezi umefikia wapi.

Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa alieleza hayo baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kudai upelelezi bado haujakamilika.

Swai aliomba apewe siku 14 kwa ajili ya kukamilisha ripoti ya polisi ya upelelezi ambayo wanasubiri.

Kwa upande wa eakili wa utetezi, Mutakyamirwa Philemon  aliomba mahakama itoe siku saba, lakini Swai alisisitiza kuomba siku 14 kama ilivyo kwenye kesi nyingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 30, 2017 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi umekamilika ama la.

 Aveva na Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha za kigeni Dola300,000 za Marekani.