Mbunge afafanua sakata la mishahara mitano hewa

Mbunge wa Makete (CCM), Profesa Norman Sigalla

Muktasari:

Profesa Sigalla alitoa maelezo hayo alipofika ofisi za gazeti hili, baada ya kudaiwa kupokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa miezi mitano wakati alikwisha acha kazi hiyo alipoteuliwa kugombea ubunge wa Makete na kushinda.

Dar es Salaam. Mbunge wa Makete (CCM), Profesa Norman Sigalla ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, amekanusha kiasi cha fedha kilichoingia kwenye akaunti yake kwamba si Sh23 milioni bali ni Sh5,091,734.96 ambazo zilikuwa hazieleweki.

Profesa Sigalla alitoa maelezo hayo alipofika ofisi za gazeti hili, baada ya kudaiwa kupokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa miezi mitano wakati alikwisha acha kazi hiyo alipoteuliwa kugombea ubunge wa Makete na kushinda.

Hali hiyo, iliyoelezwa kuisababishia Serikali hasara ya Sh23 milioni, ilitokana na madai kwamba hata baada ya kuacha kazi aliendelea kupokea mshahara wake wa ukuu wa wilaya wa Sh4.6 milioni kutokana na ofisa utumishi wa ofisi ya katibu tawala wa Mkoa wa Ruvuma kumrudisha kwenye orodha ya malipo ya mshahara.

 

Habari zaidi soma Gazeti la Mwananchi