Msigwa athibitishwa Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa

Muktasari:

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Ikulu, Peter Ilomo imeeleza kuwa Msigwa amethibitishwa kuanzia leo Agosti 31, 2016 kushika wadhifa huo.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemthibitisha Gerson Msigwa kuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Ikulu, Peter Ilomo imeeleza kuwa Msigwa amethibitishwa kuanzia leo Agosti 31, 2016 kushika wadhifa huo.

Kabla ya uthibitisho huo, Msigwa alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Rais, katika Ofisi ya Rais Ikulu kuanzia tarehe Novemba 17, 2015 aliposhika nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Salva Rweyemamu.