Wafanyabiashara wahimizwa kuheshimu mikopo
Muktasari:
Martin amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Chama cha Akiba na Mikopo (Agape Saccos) Kata ya Ubaruku.
Mbarali. Ofisa Mikopo wa Benki ya CRDB wilayani Mbarali Mkoa wa Mbeya, James Martin amewaonya wakulima na wafanyabiashara wa mpunga kuacha matumizi yasiyostahili kwa fedha za mikopo, badala yake wawekeze kwenye kilimo.
Martin amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Chama cha Akiba na Mikopo (Agape Saccos) Kata ya Ubaruku.
Martine amesema kuna tabia ya baadhi ya wakulima na wafanyabishara kukopa fedha kwa ajili ya ushindani wa michango ya harusi, starehe na kujikuta wakikwama katika urejeshaji.
“Mmefungua milango katika taasisi za fedha, viongozi mnapaswa kuwa na dhamana kwa wanachama wenu wanapohitaji mikopo kwa kutembelea miradi wanayoanzisha,” amesema.