Rais Magufuli amesema 3,004 wamejitokeza kuwania nafasi 261

Muktasari:

Nafasi hizo ni za uenyekiti wa CCM mkoa na jumuiya zake

Dar es salaam. Wagombea 3,004 wamejitokeza kuwania nafasi 261 za uenyekiti wa mikoa na jumuiya za CCM.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ambaye Rais John Magufuli hiyo imetokana na imani ya wanachama kuongezeka na kuwa kubwa.

Amesema hatua hiyo inatokana na idadi ya wagombea 3004 kati ya viongozi 261 tu wanaohitajika kupitishwa leo Jumanne katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM.

Akizungumza wa kikao hicho leo Jumanne, Rais Magufuli amesema kazi ya pitisha majina hayo ilifanyika kwa muda wa wiki mbili chini ya Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana.

"Majina ni mengi yanafika 3004 lakini wanaohitajika ni 261, hii ni tafsiri ya CCM jinsi gani inavyokubalika,” amesema Rais Magufuli.

Amesema katika kuimarisha chama hicho, wanachama watakaobaki ndani ya CCM ni waadilifu, wanaochukia ubadhirifu na siyo CCM maslahi binafsi.