Wakazi zaidi ya 100 waondolewa kwa nguvu nyumba za CDA

Muktasari:

Wamiliki hao waliondolewa na kampuni ya udalali ya Mvina, zoezi liloanza  asubuhi leo chini ya usimamizi wa polisi walikuwa na mabomu ya machozi na bunduki.

Dodoma. Wakazi zaidi ya 100 wamendolewa kwa nguvu katika  nyumba zinazomilikiwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) baada ya kukaidi agizo la kuhama kwa hiari ili kupisha ukarabati.

Wamiliki hao waliondolewa na kampuni ya udalali ya Mvina, zoezi liloanza  asubuhi leo chini ya usimamizi wa polisi walikuwa na mabomu ya machozi na bunduki.

Awali wapangaji hao walipewa notisi ya kuhama kwa hiari ya siku 90 lakini baadaye wakaongezewa wiki moja iliyoisha leo.

Baadhi ya wapangaji hao ambao hulipa kodi ya kati ya Sh 18,000 hadi 22,000 kwa mwezi kwa nyumba ya nyumba vitatu wanadaiwa madeni ya zaidi ya Sh 7 milioni.

Kwa mujibu wa CDA baada ya kukarabati huo wapangaji watakaokubali kuendelea kukaa hapa wataingia mkataba upya wa kupanga kwenye nyumba hizo.