Wanafunzi wa Lucky Vicent warejea

Muktasari:

katika ajali hiyo walifariki watu 32

Arusha .Wanafunzi watatu wa Shule ya Lucky Vincent waliokuwa wakipatiwa matibabu Marekani wamewasili nchini asubuhi hii katika Uwanja wa ndege wa KIA.

Wanafunzi hao manusura wa ajali iliyotokea mwezi wa tano wamelakiwa na umati wa watu wakiwamo Wanafunzi wenzao wa  shule ya Lucky Vicent.

Wanafunzi hao ni wale  walionusurika katika ajali iliyotokea wilayani Karatu mkoa wa Arusha na kupelekwa Marekani kwa matibabu .

Wanafunzi waliorejea ni Doreen mshana,Sadia Awadh na Wilson Tarimo