Wauaji albino kunyongwa hadi kufa

Muktasari:

Jaji Firmin Matogolo ametoa hukumu hiyo leo baada ya kuridhika na ushahidi kuwa ndio walimuua mlemavu huyo mkazi wa Wilaya ya Biharamulo mwaka 2008.

Bukoba. Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba imewahukumu kunyongwa hadi kufa watuhumiwa wawili, Pankras Minago na Lameck Bazil kwa kumuua mlemavu wa ngozi, Magdarena Andrea.

Jaji Firmin Matogolo ametoa hukumu hiyo leo baada ya kuridhika na ushahidi kuwa ndio walimuua mlemavu huyo mkazi wa Wilaya ya Biharamulo mwaka 2008.